• HABARI MPYA

    Wednesday, April 17, 2013

    CRAIG BELLAMY AIPANDISHA LIGI KUU ENGLAND CARDIF CITY BAADA YA MIAKA 51


    KAMARI inalipa. Baada ya miaka kutumia fedha kibao, kusota, vilio hadi kufika Mahakama Kuu, hatimaye Cardiff City ikiongozwa na mkongwe Craig Bellamy imefanikiwa kurejea matawi ya juu baada ya miaka 51 ya kupotea kwenye soka ya England.
    Ilikuwa ni sare ya bila kufungana jana dhidi ya Charlotn iliyowahakikishia kupanda Ligi Kuu, jambo ambalo kwa miaka ya karibuni hawakuonekana kuliweza.
    Lakini kama ulikuwa una msimu kama waliokuwa nao Cardiff, inawezekana ukasamehewa.
    Going up: Cardiff players celebrate in the changing room after getting promoted to the Premier League
    Shangwe: Wachezaji wa Cardiff wakishangilia katika chumba cha kubadilishia nguo baada ya kupanda Ligi Kuu
    Some people are on the pitch: Cardiff fans celebrate on the pitch saying goodbye to the Football League Show and welcoming being on Match of the Day
    Mchezaji wa 12 uwanjani: Mashabiki wa Cardiff wakishangilia kurejea Ligi Kuu
    I'll drink to that: Craig Bellamy downs champagne in the dressing room
    Favourite: Bellamy enjoys Cardiff's promotion to the Premier League
    Mvinyo wa furaha: Craig Bellamy akigonga shampeni kwenye chumba cha kubadilishia nguo

    VIKOSI VYA JANA

    Cardiff: Marshall, McNaughton, Turner, Barnett, Taylor, Noone (Smith 71), Kim, Gunnarsson, Mutch, Bellamy, Gestede.
    Benchi: Lewis, Whittingham, Cowie, Conway, Mason, Nugent.
    Charlton: Hamer, Solly, Morrison, Dervite, Wiggins, Harriott, Hughes (Gower 81), Jackson, Pritchard (Green 88), Kermorgant, Fuller (Obika 81).
    Benchi: Button, Taylor, Kerkar, Wilson.
    Njano: Fuller.
    Mahudhurio: 26,338
    Refa: Scott Mathieson
    Cardiff imepanda Ligi Kuu England
    Championship
    Timu hiyo imepanda baada ya kucheza mechi 43 na kufikisha pointi 84 ikiwa kileleni mwa Ligi hiyo, mbele ya Hull City yenye pointi 77, Watford 71 na Brighton & Hove Albion yenye pointi 66.
    Ilikuwa ni furaha kubwa jana kwa uongozi, wachezaji na mashabiki wa timu hiyo baada ya sare hiyo ambayo moja kwa moja inawapa tiekti ya kuingia kwenye vita na vigogo msimu ujao katika Ligi Kuu England.
    Hawatamsahau refa Scott Mathieson aliyechezesha mechi hiyo iliyowarejesha Ligi Kuu jana mbele ya mashabiki 26, 338.
    Cardiff sasa inawaachia vita ya kuwania nafasi nyingine za kupanda Hull City na Watford.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: CRAIG BELLAMY AIPANDISHA LIGI KUU ENGLAND CARDIF CITY BAADA YA MIAKA 51 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top