• HABARI MPYA

    Tuesday, August 06, 2013

    AMBAVYO WENGER HATOMSAHAU DROGBA ALIYEKATAA KUMSAINI KWA PAUNI 100,00 TU AKIWA KINDA TENA UFARANSA

    IMEWEKWA AGOSTI 6, 2013 SAA 1:37 ASUBUHI
    KAMA Arsene Wenger alihitaji ukumbusho wowote wa kosa alilofanya katika usajili akiwa kazini Arsenal, Didier Drogba alifanya hivyo Uwanja wa Emirates Jumapili.
    Mabao mawili ya Drogba ya dakika za lala salama dhidi ya Arsenal yaliyowezesha Galatasaray kubeba Kombe la Emirates yameendeleza rekodi ya mshambuliaji huyo dhidi ya The Gunners na kufika mabao 15 katika mechi 15.
    Kwamba, katika dakika 1175 ambazo Drogba amecheza dhidi ya Arsenal, amefunga wastani wa bao moja katika kila dakika 78 na sekunde 20.
    On target: Drogba's late double for Galatasaray against clinched the Emirates Cup and further improved his astonishing scoring record against Arsenal
    Alifunga: Mabao mawili ya dakika za lala salama ya Drogba aliyoifungia Galatasaray ikibeba Kombe la Emirates yameendeleza rekodi yake ya kuwafunga Arsenal
    On target: Drogba's late double for Galatasaray against clinched the Emirates Cup and further improved his astonishing scoring record against Arsenal

    REKODI YA MABAO YA DROGBA LIGI KUU DHIDI YA TOP FIVE 

    WAPINZANIMABAOMECHI ALIZOCHEZAMABAO KWA MECHI
    Arsenal8110.73
    Man City5130.38
    Spurs3140.21
    Liverpool2120.17
    Man Utd1110.09 
    Ulikuwa usiku wa pigo kwa Wenger, ambaye alikataa kumsajili Drogba kwa Pauni 100,000.
    Akiwa anachipukia nyota huyo wa Ivory Coast katika miaka yake minne Le Mans kati ya mwaka 1998 na 2002, jicho la skauti wa Wenger lilimnasa mchezaji huyo.
    Wenger alikataa kumsajili, na Drogba akahamia timu nyingine ya Ligue 1, Guingamp akiwa ana umri wa miaka 23 kwa Pauni 80,000.
    Wenger alisema mwaka 2009: "Tumemuangalia kwa umakini alipokuwa Le Mans. Siyo sisi tu tuliomuangalia. Lakini tulifikiri hawezi tayari kiasi cha kutosha.
    "Lilikuwa ni kosa, lakini ukiwa kwenye soka, kila mmoja anaweza kuelewa. Tulikuwa na Thierry Henry. Tulisema tutafuatilia maendeleo ya Drogba. Hatukuwahi kumkataa,".
    Further woe: Wenger was left disappointed as Drogba inflicted more damage on his Arsenal side
    Maumivu zaidi: Wenger aliachiwa pigo na Drogba alipoisambaratisha Arsenal yake Jumapili

    UMUHIMU WA DROGBA 

    Katika mechi 35 zilizopita za Ligi Kuu kati ya Arsenal na Chelsea, rekodi ya The Blues ikiwa na Drogba ni nzuri mno tofauti waakti hayupo.Akiwepo:   W7 D3 L1           Hayupo:    W2 D9 L13
    Mwaka 2004, kufuatia msimu wa mafanikio makubwa akiwa Marseille, Drogba alisaini Chelsea kwa ada ya Pauni Milioni 24.
    Kana kwamba hilo halikuwa pigo tosha katika jino la Wenger, Drogba aliifanyizia ile mbaya timu yake uwanjani.
    Alifunga mabao 13 katika mechi 14 dhidi ya Arsenal enzi zake akiwa Stamford Bridge, mengi kati yao akifunga katika mechi muhimu.
    Wenger alipata ahueni wakati Drogba alipoondoka Chelsea kuhamia Shanghai Shenhua mwaka jana, akisema wakati huo: "Sijui ni kiasi gani Chelsea wamempoteza, lakini hatumkumbuki. Amefanya madhara mengi dhidi yetu katika kila mechi,".
    Drogba anaweza kuwa ukingoni mwa soka yake akiwa na umri wa miaka 35 sasa, lakini kwa Emirates atabakia kukumbukwa kama kiboko ya timu ya Wenger hadi siku atakapotungika daluga zake.
    Mfaransa huyo sasa atakuwa anaomba dua Arsenal isipagwe kundi moja na Galatasaray katika Ligi ya Mabingwa katika droo inayotarajiwa kupangwa mjini Monaco Agosti 29.
    BIN ZUBEIRY INAKULETEA PICHA KUTOKA MECHI 15 ZA DROGBA DHIDI YA ARSENAL...
    Agosti 7, 2005 - Ngao ya Jamii- Chelsea 2-1 Arsenal
    Drogba opened his account against Arsenal in the 2005 Community Shield at the Millennium Stadium in Cardiff, scoring with a volley after just eight minutes
    Drogba alifungua akaunti yake ya mabao dhidi ya Arsenal mwaka 2005 katika Ngao ya Jamii Uwanja wa Millennium, Cardiff, akifunga dakika ya nane
    Drogba made it 2-0 for Chelsea in the 58th minute, curling the ball into the roof of the net
    Drogba aliifungia bao la pili katika ushindi wa 2-0 kwa Chelsea dakika ya 58
    Agosti 21, 2005 - Ligi Kuu - Chelsea 1-0 Arsenal
    A fluke goal from Drogba secured Chelsea's first Premier League win over Arsenal for almost ten years
    Drogba alifunga bao la kubahatisha na kuipa ushindi wa kwanza Chelsea katika Ligi Kuu dhidi ya Arsenal ndani ya miaka karibu 10
    Februari 25, 2007 - Fainali ya Carling- Chelsea 2-1 Arsenal
    After Theo Walcott's opener in the 12th minute at the Millennium Stadium, Drogba equalised eight minutes later
    Baada ya Theo Walcott kufunga la kwanza dakika ya 12 Uwanja wa Millennium, Drogba alisawazisha dakika nane baadaye
    Drogba headed in the winner with just six minutes remaining to clinch the Carling Cup
    Drogba alifunga la ushindi zikiwa zimesalia dakika sita na kubeba Kombe la Carling
    Machi 23, 2008 - Ligi Kuu - Chelsea 2-1 Arsenal
    After going 1-0 down at Stamford Bridge, Drogba equalised in the 73rd minute with a low drive
    Baada ya kuwa nyuma kwa 1-0 Uwanja wa Stamford Bridge, Drogba alisawazisha dakika ya 73 kwa shuti dhaifu
    Another double for Drogba as he scores an 82nd minute winner to put a dent in Arsenal's title hopes
    Mabao mengine mawili kwa Drogba, akifunga la ushindi dakika ya 82
    Aprili 18, 2009 - Nusu Fainali FA- Arsenal 1-2 Chelsea
    Drogba's 84th minute winner at Wembley put Chelsea in the final
    Bao la ushindi la Drogba dakika ya 84 Uwanja wa Wembley liliipeleka Chelsea fainali
    Novemba 29, 2009 - Ligi Kuu - Arsenal 0-3 Chelsea
    Drogba put the visitors ahead in the 41st minute as he guided Ashley Cole's cross into the top corner
    Drogba aliwafungia wageni bao la kwanza dakika ya 41 akiunganisha krosi ya Ashley Cole
    Drogba sealed the 3-0 victory at the Emirates with a 25-yard free kick late on
    Drogba alihitimisha ushindi wa 3-0 Uwanja wa Emirates kwa shiti la mita 25 la mpira wa adhabu baadaye
    Februari 7, 2010 - Ligi Kuu - Chelsea 2-0 Arsenal
    In a match that Arsenal had to win to keep their title hopes alive, Drogba opened the scoring after eight minutes
    Katika mechi ambayo Arsenal ilitakiwa kushinda kuweka hai matumaini ya ubingwa, Drogba alifunga bao la kwanza dakika ya nane
    Drogba doubled Chelsea's lead in the 23rd minute with an emphatic strike
    Drogba akaifungia la pili Chelsea dakika ya 23
    Oktoba 3, 2010 - Ligi Kuu - Chelsea 2-0 Arsenal
    Ashley Cole's near-post cross was met with a neat flick from Drogba to make it 1-0 in the 39th minute
    Krosi ya Ashley Cole karibu na nguzo ya lango ilikutana na Drogba akafunga bao la kwanza dakika ya 39
    Agosti 4, 2013 - Kombe la Emirates- Arsenal 1-2 Galatasaray
    With Arsenal just 11 minutes away from clinching the Emirates Cup, Drogba equalised with a penalty
    Zikiwa zimesalia dakika 11 Arsenal kusherehekea Kombe la Emirates, Drogba alisawazisha kwa penalti
    Drogba scored his 15th goal against Arsenal to clinch the Emirates Cup for Galatasaray, blasting home after a quality ball from Wesley Sneijder
    Drogba alifunga bao lake la 15 dhidi ya Arsenal na kutwaa Kombe la Emirates akiwa na Galatasaray, baada ya kazi nzuri ya Wesley Sneijder waliyeingia naye kipindi cha pili siku hiyo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: AMBAVYO WENGER HATOMSAHAU DROGBA ALIYEKATAA KUMSAINI KWA PAUNI 100,00 TU AKIWA KINDA TENA UFARANSA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top