• HABARI MPYA

    Thursday, August 08, 2013

    REAL MADRID YAIFUMUA CHELSEA 3-1, RONALDO AMTWANGA MOURINHO VIBAO VIWILI

    IMEWEKWA AGOSTI 8, 2013 SAA 1:57 ASUBUHI
    KIUNGO Frank Lampard alicheza kwa mara ya kwanza majira haya ya joto, lakini alishindwa kumzuia Cristiano Ronaldo kuinyanyasa Chelsea jana.
    Kabla ya mechi hiyo na Real Madrid mjini Miami, kiungo huyo mkongwe alikosa mechi zote za kujiandaa na msimu za klabu, Stamford Bridge kutokana na kuwa majeruhi.
    Lakini Lampard ameimarika na kuanza kazi tayari kwa mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu dhidi ya Hull City, Agosti 18 baada ya kumaliza dakika 45 za kwanza katika Fainali ya Mabingwa wa Kimataifa wa Guinness.
    Katika mechi hiyo, mabao mawili ya Ronaldo na moja Marcelo, yalitosha kuitotesha timu ya Jose Mourinho 3-1 dhidi ya timu yake ya zamani ambayo kwa sasa inafundishwa na Carlo Ancelotii.
    Chelsea ilipata bao lake pekee kupitia kwa Ramires.  
    Kikosi cha Real Madrid kilikuwa: Casillas, Arbeloa, Pepe, Ramos, Marcelo, Modric, Khedira, Isco, Ozil, Ronaldo na Benzema.
    Chelsea: Cech, Ivanovic, Terry, Cahill, Cole, Lampard, Van Ginkel, Ramires, Oscar, Hazard na Lukaku.
    On target: Cristiano Ronaldo scored a brace as Chelsea went down to the La Liga giants
    Kiboko yao: Cristiano Ronaldo amefunga mabao mawili dhidi ya Chelsea jana
    Party time: Real Madrid stars celebrate with the International Champions Cup after beating Chelsea
    Kujiachia: Nyota wa Real Madrid wakisherehekea na taji lao la Mabingwa wa Kimataifa wa Guinness
    Lethal: Ronaldo blasted home a free-kick and later added a header to help Madrid secure the game
    Kitu hichoo: Ronaldo akifunga kwa mpira wa adhabu
    Unloved: A Real Madrid fan holds up a banner showing he doesn't care that Mourinho left the club
    Mapenzi yameisha: Shabiki la Real Madrid likiwa limebeba bango kuonyesha kutojali kuondoka kwa Mourinho katika klabu hiyo
    Chinwag: Mourinho and former Chelsea boss, and current Madrid manager, Carlo Ancelotti, have a chat
    Mazungumzo baada ya tukio: Mourinho na kocha wa zamani wa Chelsea, ambaye kwa sasa ni kocha wa Madrid, Carlo Ancelotti wakizungumza baada ya mechi
    Triumphant: Real Madrid stars celebrate after beating Chelsea in the final of the Champions Cup
    Mabingwa: Nyota wa Real Madrid wakisherehekea kuifunga Chelsea katika fainali ya Mabingwa wa Kimataifa wa Guinness
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: REAL MADRID YAIFUMUA CHELSEA 3-1, RONALDO AMTWANGA MOURINHO VIBAO VIWILI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top