• HABARI MPYA

    Friday, August 09, 2013

    SPURS YASAINI KIUNGO LA KIMATAIFA LA UFARANSA

    IMEWEKWA AGOSTI 9, 2013 SAA 4:15 USIKU
    KLABU ya Tottenham imekamilisha uhamisho wa kiungo wa Toulouse, Etienne Capoue wa Pauni Milioni 8.6 baada ya vipimo vya afya. 
    Ada ya uhamisho wa mwasoka huyo wa kimataifa wa Ufaransa, ambaye pia alikuwa anatakiwa na Cardiff City na Atletico Madrid, unahusisha na malipo mengine.  
    Capoue, mwenye umri wa miaka 24, ni kiungo mkabaji, lakini mchezaji huyo mwenye urefu wa futi 6 na inchi 2, anaweza kucheza kama beki wa kati.
    AVB's latest signing: Etienne Capoue has joined Tottenham from Toulouse
    Usajili mpya wa AVB: Etienne Capoue amejiunga na Tottenham kutoka Toulouse
    Etienne Capoue
    Tottenham inahitaji kujiimarisha baada ya kumuuza Steven Caulker na ikiwa na inakabiliwa na tatizo la majeruhi kwa Jan Vertonghen na Younes Kaboul. 
    Capoue, ambaye amefunga mabao saba katika mechi 34 za ligi msimu uliopita, aliingia kwenye hesabu za Andre Villas-Boas tangu January na Mreno huyo amtimiza ndoto zake kumnasa.
    Tottenham bado inamuwania kiungo wa Roma, Miralem Pjanic, mwenye umri wa miaka 23, wakati majadiliano ya kuimarisha zaidi kikosi yanaendelea, akiwemo winga Jese Rodriguez, kuhusishwa katika biashara na Real Madrid juu ya Gareth Bale.
    In at the Lane: Capoue, left, seen here challenging Bordeaux's Henri Saivet, has signed for Spurs
    Capoue, kushoto, anaonekana hapa akipambana na mchezaji wa Bordeaux, Henri Saivet, amesaini Spurs
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: SPURS YASAINI KIUNGO LA KIMATAIFA LA UFARANSA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top