• HABARI MPYA

    Wednesday, August 07, 2013

    WENGER ASEMA ARSENAL WAPO MKAO WA KULA KWA SUAREZ...ANAKIMBIZANA NA MUDA KUWAHI DIRISHA LA UEFA KABLA HALIJAFUNGWA AGOSTI 12

    IMEWEKWA AGOSTI 7, 2013 SAA 2:42 USIKU
    KLABU ya Arsenal ipo katika mbio za kupambana na muda kumsajili Luis Suarez kuelekea mchezo wao wa kufuzu Ligi ya Mabingwa na kocha Arsene Wenger amesema wapo 'tayari tayari' kwa uhamisho wa mshambuliaji huyo Liverpool.
    The Gunners iliweka mezani ofa ya Pauni Milioni 40, ambayo ilikuwa inaamika itatosha kwa uhamisho wa nyota huyo wa Uruguay - lakini ikapigwa chini na klabu hiyo ya Anfield.
    Pamoja na hayo, Suarez ameweka wazi kwamba anataka kuondoka, akilalamika katika mahojiano kwamba Liverpool imekiuka ahadi ya kocha Brendan Rodgers.
    VIDEO Luis Suarez amezingirwa na mashabiki wa Liverpool
    All eyes on him: Suarez is pictured by fans heads to the 'Take a Peek' 3D baby scanning centre in St Helens
    Macho yote kwake: Suarez akipigwa picha na mashabiki alipokuwa akielekea kiruo cha watoto cha 'Take a Peek' 3D huko St Helens
    Shake on it: Suarez greets more young fans outside the centre
    Mikono: Suarez akisalimiana na mashabiki watoto nje ya kituo hicho
    At the clinic: Suarez was mobbed after he left a baby scanning clinic
    Katika kliniki: Suarez alizingirwa baada ya kuondoka katika kliniki hiyo
    Posing: Suarez stops for pictures with fans
    Pozi: Suarez alisimama kupiga picha na mashabiki
    Mini-me: Suarez's team-mates travelled to Norway, while the striker trained alone at Melwood with his daughter
    Mimi tu: Wachezaji wenzake Suarez wamekwenda Norway, wakati yeye anafanya mazoezi peke yake Melwood na binti yake
    Mini-me: Suarez's team-mates travelled to Norway, while the striker trained alone at Melwood with his daughter
    Suarez training with his daughter

    NUKUU NZITO YA SUAREZ

    'Nina miaka 26. Nataka kucheza Ligi ya Mabingwa. Nimesubiri mwaka mmoja na hakuna hata mmoja anayeweza kusema sikujitolea kitu kitu kusaka nafasi hiyo.'
    'Nina maneno ya klabu na tuliandikiana Mkataba na tutafurahi kulifikisha hili suala Bodi ya Ligi Kuu ili waamuwe kesi hii, lakini sitaki hayo yafike huko.'
    'Walinipa maneno yao mwaka uliopita na sasa nataka waheshimu hayo. Na hii si kitu ambacho kinamuhusu kocha, lakini kitu ambacho kiliandikwa kwenye Mkataba. Siendi klabu nyingine kuiumiza Liverpool.'
    GONGA HAPA USEMI HABARI KAMILI
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 - kwa sasa anatumikia adhabu ya kukosa mechi 10 kwa kumng'ata mchezaji wa Chelsea, Branislav Ivanovic mwishoni mwa msimu uliopita bado hajawasilisha barua rasmi ya kuondoka au kufungua mashitaka Bodi ya Ligi Kuu kushinikiza kuondoka.
    Kwa vyovyote Arsenal inatakiwa kuharakisha uhamisho wa Suarez kabla ya mechi zaio mbili za kufuzu Ligi ya  Mabingwa baadaye mwezi huu, kwani tarehe ya mwisho ya usajili wa michuano hiyo kwa mujibu wa UEFA ni saa 5:00 asubuhi Jumatatu ya Agosti 12.
    Wenger amesema katika mahojiano na Al Jazeera Sport kwamba wanatakiwa kukimbizana na muda kuwahi dirisha la usajili kabla halijafungwa.
    "Kwa sasa mambo yako tayari tayari. Nimesikia kwamba (Suarez anataka kuchukua hatua za kisheria kushinikiza uhamisho), lakini haya ni mambo ambayo wakati mwingine wewe mnunuzi huwezi kujihusisha nayo," alisema.
    "Hiyo hadithi baina ya Suarez na Liverpool na sijui amesema nini, nini aliahidiwa na kipi kiliandikwa na hiyo ni Suarez na Liverpool ambao wanaweza kuamua.
    "Hatuna cha kufanya. Tumeambiwa kwamba mchezaji anataka kuondoka Liverpool na hiyo ndiyo sababu tumechukua hatua. Hakika sifahamu Liverpool wataamua nini," alisema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: WENGER ASEMA ARSENAL WAPO MKAO WA KULA KWA SUAREZ...ANAKIMBIZANA NA MUDA KUWAHI DIRISHA LA UEFA KABLA HALIJAFUNGWA AGOSTI 12 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top