IMEWEKWA OKTOBA 6, 2013 SAA 2:15 USIKU
"Kwanza nachukua fursa hii kuwakaribisha na
kuwashukuru kwa kuitikia mwaliko wetu na kuja hapa leo hii kwenye shughuli hii
ya kuzindua kwenu kampeni mpya ya Kilimanjaro Premium Lager inayojulikana kama
NANI MTANI JEMBE. Natoa shukrani za kipekee kwa Mwenyekiti wa Yanga Bw. Yusuf
Manji na Mwenyekiti wa Simba, Mheshimiwa Aden Rage kwa ushirikiano wao katika
kufanikisha shughuli ya leo pamoja na kutuunga mkono katika kampeni hii
tunayoizindua leo hii.
![]() |
Mashabiki wa Simba na Yanga wakicheza |
![]() |
Meneja wa Bia ya Kilimanjaro akihutubia Leaders leo |
Kama
mnavyojua Kilimanjaro Premium Lager imekuwa mdhamini mkuu wa Simba na Yanga kwa
miaka mitano sasa tangu mwaka 2008 ambapo tulisaini mkataba kwa mara ya kwanza
na kuongeza tena mkataba wa miaka mitano mwaka 2011 ambao utadumu mpaka mwaka
2016. Lengo letu kubwa katika udhamini huu ni kuziimarisha Simba na Yanga ili
ziendelee kuwa fahari ya Watanzania kama ilivyo bia ya Kilimanjaro Premium
Lager na kuzifikisha kwenye kilele cha mafanikio. Vilevile udhamini huu
ulilenga kuitangaza bia ya Kilimanjaro Premium Lager kupitia klabu hizi kongwe
zenye historia kubwa katika taifa hili pamoja na mashabiki wengi zaidi kuliko
klabu nyingine yoyote.
Watanzania tuna sifa ya umoja na tuna jambo
moja ambalo limetuunganisha katika makundi mawili unapozungumzia soka. Bila
kujali dini wala kabila, kila Mtanzania aidha ni shabiki wa Simba au Yanga na hii
ni kutokana na historia kubwa ambayo vilabu hivi vimeijenga na pia kutokana na
sifa kubwa ambayo vilabu hivi vimeiletea Tanzania katika bara letu la Afrika
kutokana na utani wa jadi ambao ni mojawapo ya mambo yanayotutambulisha
Watanzania. Utani huu wa jadi umekuwa chachu kubwa ya maendeleo ya vilabu hivi
kwa sababu unaleta msukumo wa kila klabu kuhakikisha inajiimarisha ili
kushindana ipasavyo na kupata mafanikio. Vile vile utani huu wa jadi umeweza
kuleta msisimko wa aina yake kati ya mashabiki.
Kupitia kampeni ya NANI MTANI JEMBE, bia ya
Kilimanjaro Premium Lager imeamua kutumia utani huu wa jadi uliopo kati ya mashabiki
wa Simba na Yanga kuendelea kuwaleta pamoja mashabiki wa timu hizi kongwe na
zinazopendwa zaidi hapa nchini. NANI MTANI JEMBE inazinduliwa rasmi leo na
itadumu kwa siku 75 hadi Desemba 14 2013. Kama ambavyo mmeona kwenye vyombo vya
habari, kabla ya uzinduzi huu siku ya leo, tumetabulisha kampeni hii kwa
wafanyakazi wa TBL kwenye kiwanda cha Mwanza na kiwanda cha Arusha na vilevile
tutaitambulisha kampeni hii kwa wafanyakazi wa TBL Mbeya tarehe 11 mwezi huu.
Hii ni katika kuhakikisha wafanyakazi wanakuwa mabalozi pia wa kutangaza
kampeni hii.
ü Kama nilivyosema awali, NANI MTANI JEMBE itahusisha mashabiki wa
klabu za Simba na Yanga.
ü Kilimanjaro Premium Lager imetenga kiasi cha shilingi milioni 100
ambazo zitashindaniwa Simba na Yanga kupitia mashabiki wake.
ü Kampeni itakapoanza kila klabu itatengewa kiasi cha shilingi milioni
50.
ü Katika kipindi hicho chote mteja ambaye ni Mtani Jembe akibandua
ganda la kizibo cha bia ya Kilimanjaro Premium Lager ataona namba. Ataandika
jina la timu yake (SIMBA au YANGA) ikifuatiwa na namba hiyo ya kwenye kizibo
kasha atatuma kwenda namba 15440 na kuipa shavu timu yake. Baada ya hapo
atapata ujumbe wa kuthibitisha kwamba meseji yake imepokelewa. Kwa kufanya
hivyo atakuwa amepunguza kiasi cha shilingi 1,000 kwenye akaunti ya klabu pinzani na kuiongezea klabu yake kiasi
hicho cha sh. 1,000.
ü Mwisho wa kampeni kama mashabiki wa Simba walipiga kura zaidi na
kuichangia zaidi basi Simba itapata milioni 60 na Yanga itapata milioni 40. Na
vilevile mwisho wa kampeni kama mashabiki wa Yanga walipiga kura zaidi na
kuichangia zaidi basi Yanga itapata milioni 60 na Simba itapata milioni 40.
ü Mteja anayetuma SMS atachajiwa kiwango cha kawaida cha kutuma sms na
baada ya kutuma sms atapata sms ya uthibitisho kwamba ameipigia kura timu yake
na kufanikiwa kuichangia kiasi cha shilingi 1,000. Kutokana na upigaji kura wa
mashabiki, akiba ya timu wanayoshabikia itakuwa ikiongezeka au kupungua
kulingana upigaji kura.
Mwisho wa kampeni fedha hizo zitakabidhiwa
kwa uongozi wa kila timu kulingana na matokeo ya kura na klabu zitajiamulia
namna ya kutumia fedha hizo katika miradi yake ya maendeleo.
![]() |
Mwenyekiti wa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage akisaidiana na Katibu wake, Evodius Mtawala kuvutana na viongozi wa Yanga, Mohamed Bhinda na Lawrence Mwalusako kulia |
![]() |
Hapa wanachuana katika Futsall |
Kampeni ya Nani Mtani Jembe itawafikia
mashabiki wote wa Simba na Yanga nchi nzima kupitia matukio mbalimbali
yatakayofanyika nchi nzima na matukio hayo ni pamoja na kutembelea Matawi ya
Simba na Yanga pamoja na vijiwe vya Simba na Yanga, Bar promotions, Road shows,
Mabonanza ya kila wiki, Mashindano ya
Fussball (mpira wa mezani) na mambo mengine mengi ya kusisimua. Mashabiki
wataweza kujishindia zawadi mbalimbali zitakazotolewa kupitia matukio haya na
vilevile mashabiki watakaopiga kura wataweza kujishindia zawadi mbalimbali kila
siku zitakazokuwa kwenye vizibo vya chupa za Kilimanjaro Premium Lager.
Nyinyi kama watani wa jadi mnaozipenda
klabu zenu tunawaomba muwe mabalozi wa kampeni hii ili mwishoni tuone NANI
MTANI JEMBE. Asanteni sana kwa kunisikiliza.
Sasa nauliza, NANI MTANI JEMBE?"