Na Mwandishi Wetu, Algiers
TIMU ya taifa ya Algeria imepata ushindi wa bao 1-0 iliyouhitaji dhidi ya Burkina Faso usiku huu na kujikatia tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwakani Brazil.
Waalgeria walipata bao hilo mapema kipindi cha pili, kupitia kwa Madjid Bougherra na kufanya matokeo ya jumla yawe 3-3, baada ya awali Burina kushinda 2-0.
Algeria inaungana na Cameroon, Ivory Coast, Ghana na Nigeria kukamilisha idadi ya timu tano za Afrika.
Burkina Faso, washindi wa pili wa Kombe la Mataifa ya Afrika mapema mwaka huu, walikuwa wakipigania kushiriki Kombe la Dunia kwa mara ya kwa..
0 comments:
Post a Comment