• HABARI MPYA

    Saturday, August 02, 2014

    TAIFA STARS MAZOEZINI LEO ZIMPETO TAYARI KUMCHARANGA MAPANGA MAMBA KESHO

    Wachezaji wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kutoka kulia Khamis Mcha 'Vialli', Mrisho Ngassa na Himid Mao wakiwa mazoezini Uwanja wa Zimpeto mjini Maputo jioni ya leo, kujiandaa na mchezo wa marudiano kesho dhidi ya wenyeji Msumbiji, Mambas hatua ya mwisho kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) mwakani nchini Morocco. Stars ililazimishwa sare ya 2-2 kwenye mchezo wa kwanza na kesho kwenye Uwanja huo watahitaji ushindi wa ugenini au sare ya kuanzia mabao 3-3. Ikiwa 2-2 mshindi ataamuliwa kwa penalti.
    Thomas Ulimwengu na Erasto Nyoni wakigombea mpira
    Himid Mao kushoto na Simon Msuva kulia
    Mbwana Samatta akimiliki mpira pembeni ya Mrisho Ngassa
    Kipa Deo Munishi 'Dida' yuko tayari kwa mchezo wa kesho
    Simon Msuva akiupitia mpira miguuni mwa Khamis Mcha 'Vialli'
    Haroun Chanongo akimiliki mpira mbele ya Mbwana Samatta
    Kevin Yondan kushoto akiwania mpira dhidi ya Simon Msuva
    Kevin Yondan anaweza kuanzia benchi kesho akimpisha Aggrey Morris
    Kocha Mart Nooij kulia akisema na vijana wake 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA STARS MAZOEZINI LEO ZIMPETO TAYARI KUMCHARANGA MAPANGA MAMBA KESHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top