20 Mei, 2012 - Saa 15:01 GMT
Arjen Robben
WINGA wa Bayern Munich ambaye zamani aliichezea Chelsea,
Arjen Robben amekiri kua kukosa ule mkwaju wa penati lilikua ''balaa".
Mchezaji huyo kutoka Uholanzi alisema, sikupiga vizuri
peneti ile. Nilitaka niupige mpira na nguvu nikilenga upae kidogo lakini
haukuweza kupaa nilivyokusudia.
"siwezi kusimulia ninivyojihisi kwa maneno lakini ni
wakati mgumu kweli."
Fursa ya Robben kupiga mkwaju huo ilitokea baada ya Drogba
kumkwatua Frank Ribery ndani ya eneo la hatari, lakini Petr Cech akaokoa mpira
ule.
Robben alitulizwa kiwewe cha kukosa na kubembelezwa na
Drogba pamoja na Michel Platini baada ya mikwaju iliyomalizika kwa ushindi wa
Chelsea wa 4-3.
Robben alisema baadaye kwamba"Ukweli ni kwamba licha ya
Drogba na Platini kunipa maneno mazuri, nashukuru, lakini muhimu nilitaka
ushindi na kombe hilo.
Meneja wa Bayern Jupp Heynckes alimuunga mkono Robben
alipokataa kushiriki mikwaju ya mwisho.
0 comments:
Post a Comment