• HABARI MPYA

    Friday, June 08, 2012

    KOCHA GAMBIA TUMBO JOTO KWA STARS, AJA NA NYOTA WA REAL YA HISPANIA


    Majeruhi wakiwa nje ya mazoezi


    Nge wa Gambia wakipasha Karume jioni hii

    Benchi la Ufundi

    Bin Zubeiry kushoto akiagana na kocha Machini baada ya mahojiano Karume
    Wachezaji wa Gambia wakitoka uwanjani baada ya mazoezi 

    Kiungo wa Gambia, Saihou Gassama (18), anayechezea Real Zaragoza B ya Hispania

    KOCHA Mkuu wa Nge wa Gambia, Mtaliano, Luciano Machini amesema mechi ya Jumapili dhidi ya wenyeji Tanzania, Taifa Stars ya Kundi C kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014, itakuwa ngumu kwa sababu wapinzani wao ni wazuri.
    Akizungumza na BIN ZUBEIRY katika mazoezi ya timu hiyo jioni ya leo Uwanja wa karume, Machini aliyechukua nafasi ya aliyekuwa bosi wake, Peter Bonu Johnson, Mei mwaka huu, amesema kwamba Taifa Stars ni wazuri na wana kasi uwanjani, hivyo mechi hiyo hata wachezaji wake wanajua itakuwa ngumu.
    Alisema wao walicheza vizuri dhidi ya Morocco kwenye mechi yao ya kwanza, lakini wanaingia kwenye mechi ngumu na wenyeji Jumamosi.
    Machini aliwaongoza vijana wake kwa mazoezi mepesi jioni ya leo Uwanja wa Karume na inaonekana kama ana majeruhi wasiopungua watatu, ingawa benchi la ufundi la timu hiyo kwa ujumla limefanya siri juu ya hali za afya za wachezaji wao.
    Nge wa Gambia waliotoka sare ya 1-1 nyumbani na Morocco kwenye mechi ya kwanza Jumamosi, waliwasili nchini jana saa 5.30 usiku kwa ndege ya Kenya Airways tayari kwa mechi dhidi ya Taifa Stars, iliyofungwa 2-0 na Ivory Coast katika mechi ya kwanza ya Kundi hilo Jumamosi mjini Abidjan, itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Msafara wa timu hiyo wenye watu 31 wakiwemo wachezaji 22 unaongozwa na
    Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana na Michezo wan chi hiyo, Malang Jassey.
    Viongozi wengine ni Ofisa Utawala wa timu Modou Sowe, Kocha Luciano Machini, makocha wasaidizi Peter Bonu Johnson na Lamin Sambou, Kocha wa makipa Alhagie Marong, mtaalamu wa tiba mbadala (physiotherapist) Pa Matarr Ndow, Mtunza vifaa Sanna Bojang na Daktari wa timu Kalifa Manneh.
    Wachezaji ni Musa Camara, Abdou Jammeh, Momodou Futty Danso, Lamin Basmen Samateh, Ousman Koli, Pa Saikou Kujabi, Mustapha Kebba Jarju, Yankuba Mal Ceesay, Demba Savage, Saihou Gassama, Alieu Darboe, Momodou Ceesay, Pa Modou Jagne, Tijan Jaiteh, Bubacarr Sanyang, Christopher Allen, Musa Yaffa, Sulayman Marr, Mamut Saine, Hamsa Barry, Ali Sowe, Omar Colley na Saloum Faal.
    Baada ya mazoezi ya leo, Nge hao, watafanya tena mazoezi yao kesho asubuhi Uwanja wa Karume na jioni Uwanja wa Taifa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KOCHA GAMBIA TUMBO JOTO KWA STARS, AJA NA NYOTA WA REAL YA HISPANIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top