• HABARI MPYA

    Friday, June 08, 2012

    MAYAY AANDALIWA PINGAMIZI YANGA


    'Meja' Ally Mayay Tembele

    PINGAMIZI linaandaliwa na kambi ya mmoja wa wagombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Yanga, dhidi ya mgombea wa nafasi hiyo, Ally Mayay Tembele, beki na Nahodha wa zamani wa klabu hiyo.
    Habari za ndani ambazo BIN ZUBEIRY imezipata leo, zimesema kwamba kambi hiyo inataka kuwasilisha pingamizi kwa Kamati ya Uchaguzi, kupinga ‘Meja wa Soka’, Mayay kugombea nafasi yoyote Yanga, kwa sababu uchaguzi utakaofanyika Julai 15, mwaka huu ni wa kujaza nafasi za viongozi waliojiuzulu, akiwemo Mayay mwenyewe.
    “Mayay alikuwa kiongozi Yanga, akajiuzulu. Kutokana na wajumbe wengine pia kujiuzulu, akiwemo Mwenyekiti na Makamu wake, safu ya uongozi ikawa inapwaya, ndipo TFF (Shirikisho la Soka Tanzania) ikaagiza ufanyike uchaguzi kujaza nafasi. Viongozi alioingia nao madarakani Ally ambao hawajajiuzulu kama Mohamed Bhinda, bado wapo.
    Sasa iweje Mayay agombee tena? Huku ni kuchezea Katiba ya klabu. Maana yake hata gharama ambazo klabu inaingia kwa kurudia uchgauzi, yeye hazizingatii,”alisema mtoa habari huyo, leo.
    Juhudi za kumpata Mayay kuzungumzia suala hilo hazikufanikiwa kwa haraka, inagwa bado BIN ZUBEIRY inamtafuta na akipatikana tutapandisha maelezo yake.
    Katika uchaguzi huo, Yussuf Mehboob Manji atachuana na John Jambele, Edgar Chibura na Sarah Ramadhani kwenye nafasi ya uenyekiti, wakati wapinzani wa Mayay ni Ayoub Nyenzi, Yono Kevela na Clement Sanga.
    Ally Mayay wa pili kutoka kushoto waliochuchumaa katika kikosi cha Yanga cha mwaka 2001, wa kwanza kushoto wake ni Said Maulid Maulid 'SMG'. Anayemfuatia Mayay kulia kwake ni kipa Doyi Moke, Edibily Lunyamila na Yahya Issa. Waliosimama kutoka kulia ni beki Chibe Chibindu, Waziri Mahadhi, Abubakar Mohamed 'Phantom', Iddi Moshi 'Mnyamwezi', Abdulkadir Mohamed 'Tashi' na Mwanamtwa Kihwelo 'Dally Kimoko'. 
    Katika nafasi za Ujumbe waliorudisha ni Lameck Nyambaya, Ramadhani Mzimba ‘Kampira’, Mohamed Mbaraka, Ramadhani Said, Edgar Fongo, Beda Simba, Ahmad Gao, Mussa Katabaro, George Manyama, Aaron Nyanda, Abdallah Bin Kleb, Omary Ndula, Shaaban Katwila, Jumanne Mohamed Mwammenywa, Abdallah Mbaraka, Peter Haule, Justin Baruti na Abdallah Sharia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAYAY AANDALIWA PINGAMIZI YANGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top