KIUNGO mahiri wa Yanga, Haruna Niyonzima 'Fabregas' ameushawishi uongozi wa timu hiyo kumsainisha straika Meddy Kagere anayemaliza mkataba na timu ya Polisi ya Rwanda. Gazeti la Mwanaspoti limeandika jana kwamba Fabregas, ambaye alitamba na Yanga msimu uliopita amezungumza na viongozi wanaowezesha usajili wa Jangwani na kuwaambia kuwa Kagere ni bonge la straika na anaweza kufanya kazi kubwa msimu ujao. Kiungo huyo alizungumza na Mwanaspoti kutoka Lagos, Nigeria ambako timu yake ya Rwanda itacheza na Super Eagle leo Jumamosi na kusema; "Kagere ni straika mzuri sana nimekaa naye timu ya taifa namuona anavyocheza ni aina ya mchezaji ambaye Yanga inastahili kuwa naye." "Viongozi wa Yanga wamezungumza naye na mambo yanakwenda vizuri, nadhani tukirudi Rwanda wanaweza kumalizana naye. Ni mchezaji mwenye juhudi sana anayeweza kupunguza tatizo la mabao hapo Yanga, ana juhudi sana halafu si mtu wa kukubali kushindwa kirahisi. "Akifanya kazi kwa uwezo wake wote ninaoujua mimi, tutafika mbali na atang'ara sana na Yanga hata kwenye ligi ya Tanzania atakubalika upesi sana, ngoja akifanikiwa kuja utakubali maneno yangu," alisema Fabregas. Mmoja wa viongozi wa jopo la usajili alikiri kuwa Fabregas amewahakikishia wakimsajili mchezaji huyo wameula na atafanya kazi. Aliongeza kuwa bado wanaendelea na mazungumzo ya kupata beki wa kati kutoka kwenye timu ya taifa ya Kenya au Uganda na mkakati mwingine ni kuhakikisha wanamalizana na Kagere ambaye aliwahi kuitolea nje Gor Mahia ya Kenya. Ingawa tayari wametua Dar es Salaam, lakini Yanga imepanga kuachana na mastraika wake Davies Mwape wa Zambia na Kenneth Asamoah wa Ghana ili kusajili wapya wawili kutoka nje; Kagere akiwa miongoni. Simon Msuva wa Moro United ndiye straika pekee mzalendo ambaye Yanga imeshamsajili hadi sasa safari hii. |
Nick Kyrgios apologises to Rafael Nadal after forging tennis great's
signature and costing him thousands
-
Australian firebrand Nick Kyrgios has revealed the way he got back at
Rafael Nadal following his loss to the tennis legend at the 2017 China Open
final.
47 minutes ago
0 comments:
Post a Comment