• HABARI MPYA

    Monday, October 01, 2012

    MTIBWA WATOA KICHAPO CHAMAZI, WAIRUKA YANGA KWENYE MSIMAMO WA LIGI

    Wachezaji wa Mtibwa

    Na Prince Akbar
    MTIBWA Sugar ya Morogoro wamezinduka katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 kwenye Uwanja Chamazi, Dar es Salaam,  dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani.
    Mechi hiyo ilitakiwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi lakini kwa sababu ya kuonyeshwa moja kwa moja na Televisheni ya Super Sport ya Afrika Kusini imechezwa Uwanja wa Azam.
    Katika mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua, mabao ya Wakata Miwa wa Manungu, yalitiwa kimiani na Hussein Javu dakika ya 13, Awadh Juma dakika ya 16 na Shaaban Nditi dakika ya 62, wakati ya Ruvu yalifungwa na Paul Ndauka dakika ya 30 kwa  penalti na Abrahman Mussa dakika ya 64.
    Ushindi huo, unaifanya Mtibwa ifikishe pointi saba na kupanda hadi nafasi ya tatu, wakati Ruvu inabakia ‘danger zone’.
    Katika mchezo wa jana wa ligi hiyo, Yanga ilishinda mabao 3-1 dhidi ya African Lyon Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, shukrani kwake kiungo anayecheza kwa nadra kwenye timu hiyo, Nizar Khalfan aliyefunga mabao ya ushindi dakika ya 65 na 88, akitokea benchi kuchukua nafasi ya Frank Domayo.
    Nizar alifunga bao la pili, sekunde chache baada ya Benedictor Mwamlangala kuisawazishia African Lyon bao lililodumu tangu dakika ya 17, baada ya Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ kutangulia kufunga dakika ya 17.
    Ushindi huo, uliifanya Yanga ifikishe pointi saba, baada ya kucheza mechi nne na kupanda hadi nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi, ikiwa inalingana na Coastal kwa pointi na wastani wa mabao, ingawa Coastal wako nyuma kwa mechi moja, ingawa kwa matokeo ya leo, inashuka hadi nafasi ya tano.
    Simba juzi iliichapa Prisons ya Mbeya iliyorejea Ligi Kuu msimu huu mabao 2-1, yaliyotiwa kimiani na Felix Mumba Sunzu na Mrisho Ngassa, wakati la Prisons lilifungwa na Elias Maguri.
    Simba bado inaongoza ligi hiyo, kwa pointi zake 12, ikifuatiwa na Azam iliyoifunga JKT Ruvu 3-0 Ijumaa, mabao ya John Bocco ‘Adebayor’, Kipre Herma Tchetche na Kipre Michael Balou yenye pointi 10.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MTIBWA WATOA KICHAPO CHAMAZI, WAIRUKA YANGA KWENYE MSIMAMO WA LIGI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top