• HABARI MPYA

    Tuesday, April 16, 2013

    BABU MFARANSA AKALIA KUTI KAVU SIMBA SC


    Na Prince Akbar
    KWA asilimia 80, Simba itaachana na kocha Mfaransa, Patrick Liewig baada ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kutokana na sababu mbili kubwa, BIN ZUBEIRY inakuhafamisha.
    Habari kutoka ndani ya Simba SC, zimesema kwamba, kwa kuwa kuna dalili za klabu hiyo kukosa nafasi yoyote ya kuiwakilisha nchi kwenye michuano ya Afrika mwakani, hakutakuwa na sababu ya kuwa na kocha wa kigeni msimu ujao, anayelipwa mshahara mkubwa.
    Kocha Liewig kulia akiwa na baadhi ya wachezaji wake

    REKODI YA LIEWIG SIMBA SC:
                            P W D L GF GA   GD  Pts
    Simba 22 7 8 7 28 27    1 29

    MECHI ZA SIMBA CHINI YA LIEWIG:
    Simba SC 4-2 Jamhuri     (Kombe la Mapinduzi)
    Simba SC 1-1 Tusker FC (Kombe la Mapinduzi)
    Simba SC 1-1 Bandari      (Kombe la Mapinduzi)
    Simba SC 0-1 U23 Oman (Kirafiki)
    Simba SC 1-3 Qaboos      (Kirafiki)
    Simba SC 2-1 Ahly Sidab  (Kirafiki)
    Simba SC 0-1 Black Leopard (Kirafiki)
    Simba SC 3-1 African Lyon (Ligi Kuu)
    Simba SC 1-1 JKT Ruvu    (Ligi Kuu)
    Simba SC 1-1 JKT Oljoro (Ligi Kuu)
    Simba SC 0-1 Recreativo de Libolo (Ligi ya Mabingwa)
    Simba SC 1-0 Prisons v        (Ligi Kuu)
    Simba SC 0-1 Mtibwa Sugar (Ligi Kuu)
    Simba SC 0-4 Recreativo de Libolo (Ligi ya Mabingwa) 
    Simba SC 2-1 Coastal Union (Ligi Kuu)
    Simba SC 1-0 CDA       (Kirafiki)
    Simba SC 4-0 Singida United (Kirafiki)
    Simba SC 1-1 Rhino FC       (Kirafiki)
    Simba SC 0-1 Kagera Sugar   (Ligi Kuu)
    Simba SC 2-2 Toto Africans    (Ligi Kuu)
    Simba SC 1-1 Shinyanga United (Kirafiki)
    Simba SC 2-2 Azam FC (Ligi Kuu)

    Lakini pia, inaelezwa Simba SC wangevumilia kuendelea na Mfaransa huyo, anayelipwa dola za Kimarekani 5,000 kwa mwezi (zaidi ya Sh. Milioni 8 za Tanzania) kama asingekuwa na matatizo kadha wa kadhaa.
    “Hapa alipo amekwishagombana na wachezaji wengi, wengine kwa sababu na wengine bila sababu za msingi. Lakini pia, amegombana hadi na sisi viongozi. Ni mtu ambaye tumeona hatuwezi kuendelea kufanya naye kazi,”alisema kiongozi mmoja wa Simba SC.
    Lakini inaonekana wapo baadhi ya viongozi ndani ya Simba SC wanavutiwa na utendaji wa Liewig pamoja na falsafa zake na wana matumaini naye makubwa.
    Liewig ambaye ni kocha wa zamani wa akademi ya PSG ya Ufaransa, anaonekana kuamini zaidi juu ya wanasoka vijana na anataka kujenga Simba SC ya hivyo.
    Pamoja na kuikuta Simba SC inaundwa na wachezaji wazoefu wenye majina makubwa katika soka ya Tanzania, lakini Mfaransa huyo hivi sasa anatumia vijana wengi aliowapandisha kutoka kikosi cha pili.
    Ni vijana hao hao, waliokaribia kuifunga Azam FC Jumapili baada ya kuongoza 2-0, 2-1 na baadaye 2-2 katika mchezo wa juzi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 
    Hadi sasa, Liewig amekwishaiongoza Simba SC katika mechi 22, akiiwezesha kushinda saba, sare nane na kufungwa saba tangu aanze kazi Januari mwaka huu, akirithi mikoba ya Mserbia, Profesa Milovan Cirkovick. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: BABU MFARANSA AKALIA KUTI KAVU SIMBA SC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top