• HABARI MPYA

    Monday, April 15, 2013

    SASA MAN UNITED PUA NA MDOMO NA SAINI YA FALCAO

    KLABU ya Manchester United ilimshuhudia Radamel Falcao akiifungia mabao mawili Atletico Madrid Jumapili usiku na inafahamika Sir Alex Ferguson anamtaka mshambuliaji huyo.
    BIN ZUBEIRY ilinadika wiki iliyopita kwamba Ferguson anataka kutumia Pauni Milioni 47 - ambazo zitahusisha na kubadilishana na Javier Hernandez ili kumnasa mkali huyo wa mabao wa Colombia.
    Wakati United inashinda 2-0 dhidi ya Stoke, Ferguson alimpeleka msaka vipaji wake mkuu, Jim Lawlor kumuangalia Falcao akifunga mabao mawili katika ushindi wa 5-0 nyumbani dhidi ya Granada.
    Kaangalie video chini
    Wanted: Radamel Falcao (left) in action during Atletico Madrid's victory over Granada
    Anatakiwa: Radamel Falcao (kushoto) akiichezea Atletico Madrid ikiifunga Granada

    Manchester City na Chelsea zote nazo zimehusishwa kwa kiasi kikubwa kuwania saini ya Falcao, ambaye amejijengea jina kama mmoja wa wapachika mabao hodari duniani, kwa kuifungia mabao 56 Atletico tangu ajiunge nayo akitokea Porto mwaka 2011. 
    Lakini United imepiga hatua kubwa katika kuwania saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27, ikijiandaa kumuacha Hernandez ahamie Madrid kama sehemu ya dili hilo.
    On his way? Javier Hernandez in action against Stoke on Sunday - but he could be off
    Anaondoka? Javier Hernandez akiichezea United dhidi ya Stoke Jumapili, lakini anaweza kuondoka

      VIDEO  Angalia mabao bora ya Falcao
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: SASA MAN UNITED PUA NA MDOMO NA SAINI YA FALCAO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top