• HABARI MPYA

    Tuesday, April 16, 2013

    JUVE YAZIDI KUPAA ITALIA


    KLABU ya Juventus imepiga hatua kubwa katika mbio za uibingwa wa Italia, Serie A baada ya jana usiku kujitania kileleni kwa pointi 11 zaidi kufuatia mabao mawili ya Arturo Vidal kuwapa ushindi wa 2-0 dhidi ya Lazio.
    Vidal aliwafungia Juve kwa penalti baada ya Lorik Cana kumuangusha Claudio Marchisio kwenye eneo la hatari dakika ya nane.
    Spot on: Arturo Vidal scores with an early penalty for Juventus
    Mkwaju nyavuni: Arturo Vidal akifunga kwa penalti
    Happy days: Vidal celebrates with Claudio Marchisio and Stephan Lichtsteiner
    Siku za furaha: Vidal akishangilia na Claudio Marchisio na Stephan Lichtsteiner

    Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Chile, Vidal alifunga bao la pili dakika 20 baadaye akimalizia pasi ya Mirko Vucinic.
    Ikiwa imebakiza mechi sita, Juve ina pointi 74 wakiiacha mbali Napoli katika nafasi ya pili. AC Milan yenye pointi 59 ni ya tatu.
    "Ushindi huu ni muhimu sana sana kwa kutuwezesha kuzidi kupiga hatua kuelekea kwenye ubingwa,"alisema kocha Antonio Conte.
    "Bado tunahitaji pointi saba na hatutazungumza hadi tumbebe mwali,"aliongeza.
    At the double: Vidal puts Juventus 2-0 ahead
    La pili: Vidal akiifungia Juventus bao la pili
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: JUVE YAZIDI KUPAA ITALIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top