• HABARI MPYA

    Wednesday, July 17, 2013

    CHELSEA WAIPA UNITED JUAN MATA AU DAVID LUIZ NA PAUNI MILIONI 10 JUU WAPEWE ROONEY...LAKINI MASHETANI WEKUNDU WATOA NJE KIKUDA

    IMEWEKWA JULAI 17, 2013 SAA 7:13 MCHANA
    KLABU ya Manchester United imekataa ofa ya kwanza ya Chelsea kwa ajili ya Wayne Rooney - Pauni Milioni pamoja na mchezaji.
    BIN ZUBEIRY inafahamu wachezaji wawili walioambatanishwa katika ofa hiyo United ichagua mmoja ni Mchezaji Bora wa Mwaka, Juan Mata au beki Mbrazil, David Luiz.
    United imesema Rooney hauzwi na kocha wa Chelsea, Jose Mourinho sasa lazima aamue kuweka gungu tu la maana la fedha mezani.
    Something on your mind? Wayne Rooney arrives at Manchester United's training ground on Wednesday
    Lolote mawazoni mwako? Wayne Rooney akiwasili viwanja vya mazoezi vya Manchester United leo kwa mazoezi

    Arsenal pia imetoa ofa ya awali ingawa pia imetoa ofa kwa Luis Suarez na Gonzalo Higuain.Klabu hiyo ya Stamford Bridge imeonywa, isithubutu kurejea na ofa ya pili, kwani United haina mpango wa kumuuza Rooney kwa klabu nyingine ya Ligi Kuu England.
    Mourinho yu tayari kuwauza Mata na Luiz, ili fedha atakazopata kutokana na mauzo ya wawili hayo atumie kumnunua mchezaji wa United.
    Rooney anafikiri amefikia kilele cha mustakabali wake na hana zaidi cha kuthibitisha baada ya misimu tisa Old Trafford.
    Inafahamika mshambuliaji huyo wa England amechanganyikiwa na kukerwa na maneno ya kocha mpya, David Moyes kwamba hatauzwa sababu ndiye mbadala wa mshambuliaji chaguo la kwanza, Robin van Persie.
    Up for grabs? Chelsea have offered Juan Mata (above) or David Luiz (below) in part-exchange for Rooney
    Chelsea imewaofa United Juan Mata (juu) au David Luiz (chini) pamoja na Pauni Milioni 10 wapewe Rooney
    David Luiz
    Mourinho aliwasha moto jana katika jitihada zake za kuwania saini ya Rooney kwa kutoa onyo kwamba, matumaini ya England yatakuwa madogo Kombe la Dunia kama mchezaji huyo atabakia United. 
    Chelsea imehamishia nguvu zake kwa Rooney baada ya wachezaji iliyokuwa inawataka awali kuwakosa wote, Radamel Falcao amekwenda Monaco na Edinson Cavani katua PSG, zote za Ufaransa.
    Mourinho alisema: "Ikiwa Wayne ni chaguo la pili kwa Manchester United, kisha timu ya taifa itaathirika.’

    HII NDIYO SABABU CHELSEA INAWATOA JUAN MATA AU DAVID LUIZ?

    Juan Mata
    Umri: Miaka 25
    Nafasi: Kiungo mshambuliaji
    Klabu za awali: Real Madrid B, Valencia
    Takwimu za Chelsea:
    2011-12: Mechi: 54 Mabao: 12 Pasi za mabao: 23
    2012-13: Mechi 64 Mabao 20 Pasi za mabao 35 
    Hispania: Mechi: 29 Mabao 8.
    VIDEO: Mabao matamu ya Juan Mata Chelsea 
    David Luiz
    Umri: Miaka 26
    Nafasi: Beki/Kiungo
    Klabu za awali: Vitoria, Benfica
    Takwimu za Chelsea:
    2010-11: Mechi:12 Mabao: 2
    2011-12: Mechi 40 Mabao 3
    2012-13: Mechi 57 Mabao 7
    Brazil: Mechi 28 Hajafunga.







    VIDEO: Bao tamu la David Luiz dhidi ya Basle katika Europa League 



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: CHELSEA WAIPA UNITED JUAN MATA AU DAVID LUIZ NA PAUNI MILIONI 10 JUU WAPEWE ROONEY...LAKINI MASHETANI WEKUNDU WATOA NJE KIKUDA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top