• HABARI MPYA

    Friday, July 05, 2013

    HIGUAIN SASA HATARINI KUOTA MBAWA ARSENAL, GAZETI HISPANIA LAFICHUA UKWELI WA SAGA ZIMA...MBONA MAJANGA LONDON!

    IMEWEKWA JULAI 5, 2013 SAA 12:00 JIONI
    KLABU ya Arsenal sasa inakabiliwa mpambano mkali ili kumnasa Gonzalo Higuain kutoka Real Madrid, baada ya taarifa nchini Hispania kusema kwamba vigogo hao wa Hispania watataka ada kubwa ya uhamisho wa nyota huyo wa Argentina.
    Licha ya tetesi kuenea kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 yuko njiani kutua Kaskazini mwa London, gazeti la Marca limesema hakukuwa na makubaliano baina ya klabu hizo mbili, maana yake zoezi la muda mrefu la uhamisho wa nyota hiyo linaendelea.
    Ready or not? Higuain's seemingly impending move to Arsenal keeps running on
    Tayari au hapana? Sakata la Higuain kuhamia Arsenal bado bichi
    Ready or not? Higuain's seemingly impending move to Arsenal keeps running on
    Kuwasili kwa Carlo Ancelotti kama kocha wa Real kulifikiriwa kungefungua milango ya uhamisho huo, lakini gazeti la Hispania limesema Higuain zaidi anaweza akabaki Bernabeu.
    Bei ya Pauni Milioni 23 iliyotajwa, inafikiriwa ni uzushi kwani vigogo hao wa Hispania hawajataja bei rasmi ya kumuuza mwanasoka huyo wa kimataifa wa Argentina, ambayo inaweza kuwa pigo kwa Arsene Wenger.
    Baba yake Higuain alisema mapema wiki hii kwamba uhamisho huo unaweza kukamilika muda si mrefu, lakini taarifa za Hispania zinasema Real inaweza kuamua kubaki na mshambuliaji huyo. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: HIGUAIN SASA HATARINI KUOTA MBAWA ARSENAL, GAZETI HISPANIA LAFICHUA UKWELI WA SAGA ZIMA...MBONA MAJANGA LONDON! Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top