Na Mahmoud Zubeiry, Johannesburg, Afrika Kusini
IMEWEKWA AGOSTI 9, 2013 SAA 8:30 MCHANA
AZAM FC leo imepoteza mechi yake ya pili katika ziara yake ya Afrika Kusini baada ya kufungwa mabao 2-1 na Orlando Pirates, kwenye Uwanja wa Randy mjini Johannesburg, nchini hapa.
Bao pekee la Azam katika mchezo wa leo lilifungwa na kiungo Jabir Aziz dakika ya 62, wakati wenyeji walipata mabao yao mapema tu dakika ya nne na ya nane. Awali mchezo huo ulikuwa uchezwe kesho, lakini wenyeji wakaomba uchezwe leo. Na taarifa za awali jana zilikuja mechi itachezwa jioni, lakini asubuhi ya leo Azam FC wakaambiwa wanatakiwa kwenda uwanjani.
Kocha Stewart Hall aliwaamsha wachezaji wake haraka na kuwapakia kwenye basi kwenda uwanjani.
Wazi Azam iliathiriwa na kushitukizwa na kujikuta wanafungwa mabao ya mapema tu, mawili ndani ya dakika ya nane- lakini baada ya wachezaji kutulia, Orlando Pirates walikiona cha moto.
Kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’ alitawala sehemu ya kiungo vizuri na John Bocco ‘Adebayor’ aliendelea kupoteza nafasi na hata Gaudence Mwaikimba alipompokea kipindi cha pili, hakuweza kufunga.
Kipre Tchetche aliiinyanyasa mno ngome ya Pirates, lakini hakuweza kufunga tu. Beki Mkenya Jaockins Atudo ambaye sasa anahimishiwa kulia kutoka katikati, alitia krosi nyingi nzuri.
Pamoja na kufungwa mabao mawili ya haraka yaliyotokana na makosa ya Kipre Balou na Ibrahim Mwaipopo, lakini kipa Mwadini Ally alidaka vizuri. Mwadini anaweka rekodi ya kufungwa mabao matano katika mechi mbili alizodaka hapa, kwani ni yeye ndiye aliyesimama langoni timu ikifungwa 3-0 Kazier Chiefs.
Kipa wa pili, Aishi Manula alidaka wakati Azam ikishinda 1-0 dhidi ya Mamelodi.
IMEWEKWA AGOSTI 9, 2013 SAA 8:30 MCHANA
AZAM FC leo imepoteza mechi yake ya pili katika ziara yake ya Afrika Kusini baada ya kufungwa mabao 2-1 na Orlando Pirates, kwenye Uwanja wa Randy mjini Johannesburg, nchini hapa.
Bao pekee la Azam katika mchezo wa leo lilifungwa na kiungo Jabir Aziz dakika ya 62, wakati wenyeji walipata mabao yao mapema tu dakika ya nne na ya nane. Awali mchezo huo ulikuwa uchezwe kesho, lakini wenyeji wakaomba uchezwe leo. Na taarifa za awali jana zilikuja mechi itachezwa jioni, lakini asubuhi ya leo Azam FC wakaambiwa wanatakiwa kwenda uwanjani.
![]() |
Baridi kali; Benchi la Azam katika mechi leo |
PROGRAMU YA AZAM AFRIKA KUSINI:
AGOSTI 3, 2013:
Kuwasili J’burg kutoka Dar
AGOSTI 4, 2013:
Mazoezi (Chuo Kikuu cha Wits)
AGOSTI 5, 2013:
Azam 0-3 Kaizer Chiefs
AGOSTI 6, 2013: Mazoezi (Chuo Kikuu cha Wits)
AGOSTI 8, 2013:
Mazoezi (Chuo Kikuu cha Wits)
AGOSTI 10, 2013: Mazoezi (Chuo Kikuu cha Wits)
AGOSTI 11, 2013:
Mazoezi (Chuo Kikuu cha Wits)
AGOSTI 12, 2013:
Azam Vs Moroka Swallows
AGOSTI 13, 2013: Kuondoka Johannesburg kurejea Dar es Salaam
Kuwasili J’burg kutoka Dar
AGOSTI 4, 2013:
Mazoezi (Chuo Kikuu cha Wits)
AGOSTI 5, 2013:
Azam 0-3 Kaizer Chiefs
AGOSTI 6, 2013: Mazoezi (Chuo Kikuu cha Wits)
AGOSTI 7, 2013:
Azam 1-0 Mamelodi Sundwons AGOSTI 8, 2013:
Mazoezi (Chuo Kikuu cha Wits)
AGOSTI 9, 2013:
Azam 1-2 Orlando PiratesAGOSTI 10, 2013: Mazoezi (Chuo Kikuu cha Wits)
AGOSTI 11, 2013:
Mazoezi (Chuo Kikuu cha Wits)
AGOSTI 12, 2013:
Azam Vs Moroka Swallows
AGOSTI 13, 2013: Kuondoka Johannesburg kurejea Dar es Salaam
Kocha Stewart Hall aliwaamsha wachezaji wake haraka na kuwapakia kwenye basi kwenda uwanjani.
Wazi Azam iliathiriwa na kushitukizwa na kujikuta wanafungwa mabao ya mapema tu, mawili ndani ya dakika ya nane- lakini baada ya wachezaji kutulia, Orlando Pirates walikiona cha moto.
Kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’ alitawala sehemu ya kiungo vizuri na John Bocco ‘Adebayor’ aliendelea kupoteza nafasi na hata Gaudence Mwaikimba alipompokea kipindi cha pili, hakuweza kufunga.
Kipre Tchetche aliiinyanyasa mno ngome ya Pirates, lakini hakuweza kufunga tu. Beki Mkenya Jaockins Atudo ambaye sasa anahimishiwa kulia kutoka katikati, alitia krosi nyingi nzuri.
Pamoja na kufungwa mabao mawili ya haraka yaliyotokana na makosa ya Kipre Balou na Ibrahim Mwaipopo, lakini kipa Mwadini Ally alidaka vizuri. Mwadini anaweka rekodi ya kufungwa mabao matano katika mechi mbili alizodaka hapa, kwani ni yeye ndiye aliyesimama langoni timu ikifungwa 3-0 Kazier Chiefs.
Kipa wa pili, Aishi Manula alidaka wakati Azam ikishinda 1-0 dhidi ya Mamelodi.