• HABARI MPYA

    Friday, August 02, 2013

    MKALI WA MABAO UFARANSA ATUA NEWCASTLE

    IMEWEKWA AGOSTI 2, 2013 SAA 12:55 JIONI
    KLABU ya Newcastle inajiandaa kukamilisha usajili wao wa kwanza mwishoni mwa dirisha baada ya kukubali kumsajili mshambuliaji wa Lyon, Bafetimbi Gomis.
    Uhamisho wa Gomis kutua The Magpies utakamailishwa na Mkurugenzi wa Sika, Joe Kinnear, huku dili likiwa katika mwelekeo wa kufanikiwa kwa mujibu wa Rais wa klabu hiyo ya Ufaransa, Jean-Michel Aulas.
    Newcastle italipa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 8.7 kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27, ambaye alifunga mabao 16 Lyon msimu uliopita, Aulas aliliambia gazeti Le Journal du Dimanche la Ufaransa.
    First man in: Lyon striker Bafetimbi Gomis is on the brink of sealing a move to Newcastle
    Mtu wa kwanza ndani: Mshambuliaji wa Lyon, Bafetimbi Gomis yuko njiani kutua Newcastle
    Unchanged: Gomis is set to become Toon boss Alan Pardew's first signing of the summer
    Habadiliki: Gomis anatarajiwa kuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na kocha wa Toon, Alan Pardew majira haya ya joto
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MKALI WA MABAO UFARANSA ATUA NEWCASTLE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top