• HABARI MPYA

    Monday, August 05, 2013

    SOLDADO AKAMILISHA USAJILI WA REKODI SPURS

    IMEWEKWA AGOSTI 5, 2013 SAA 4:11 USIKU
    KLABU ya Tottenham imekamilisha usajili wa rekodi wa Roberto Soldado kutoka Valencia baada ya mchezaji huyo kufuzu vipimo vya afya. 
    Baada ya kubebwa na mabao ya Gareth Bale msimu uliopita, kocha wa Spurs, Andre Villas-Boas amefanya usajili wa mchezaji kipaumbele chake majira haya ya joto na sasa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28, Soldado anaanza kazi White Hart Lane  baada ya kukamilisha usajili mchana wa leo. 
    Muuwaji huyo wa Hispania, ambaye amefunga mabao 30 katika mechi 46 alizoichezea Valencia msimu uliopita, ameigharimu Tottenham Pauni Milioni 26- jambo linalomfanya awe mchezaji ghali wa klabu hiyo kihistoria. 
    Getting shirty: Soldado poses in the new Tottenham strip at the club's training ground
    Amepewa jezi: Soldado akiwa na jezi ya Tottenham katika viwanja vya mazoezi Flying high: Robert Soldado has completed his £26milllion switch to Tottenham
    Akionyesha jezi: Robert Soldado amekamilisha usajili wa Pauni Milioni 26 kutua Tottenham
    Flying high: Robert Soldado has completed his £26milllion switch to Tottenham
    New arrival: The Spaniard becomes Tottenham's record signing after completing a £26m move
    Mtu mpya:  Mspanyola aliyeweka rekodi ya mchezaji ghali Tottenham
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: SOLDADO AKAMILISHA USAJILI WA REKODI SPURS Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top