IMEWEKWA OKTOBA 7, 2013 SAA 6:24 MCHANA
KLABU ya Manchester United imempa Adnan Januzaj ofa ya mshara wa Pauni 60,000 kwa wiki ili abaki Old Trafford baada ya kuisaidia timu hiyo kushinda Uwanja wa Light.
KLABU ya Manchester United imempa Adnan Januzaj ofa ya mshara wa Pauni 60,000 kwa wiki ili abaki Old Trafford baada ya kuisaidia timu hiyo kushinda Uwanja wa Light.
Kinda huyo mwenye umri wa miaka 18, zao lingine la kizazi cha dhahabu cha Ubelgiji, alicheza mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu ya England na kufunga mabao mawili yalioyomfariji kocha David Moyes kwa ushindi wa 2-1.
Na wakati mkataba wa mshambuliaji huyo unamalizika miezi nane ijayo, klabu kadhaa zimeonyesha nia ya kumsajili, hivyo kocha huyo United anataka kumbakiza nyoa wake huyo mpya.
Kifaa: Manchester United imempa Adnan Januzaj ofa ya mshahara wa Pauni 60,000 wiki abaki katika klabu hiyo
Mitaa ya mjini: Januzaj akitalii mitaa ya Jiji la Manchester Jumapili
Kazi nzuri imefanyika: Januzaj akipongezwa na wenzake Robin van Persie na Michael Carrick baada ya kufunga
Wanamkubali: Wayne Rooney ni shabiki mkubwa wa nyoa huyo mwenye kipaji
Anamkubali kijana: Kocha wa United, David Moyes amempa nafasi Januzaj kung'ara kama alivyofanya kwa Rooney alipokuwa naye Everton
VIPAJI BABU KWA KIBLEJIGI
BIN ZUBEIRY inakutajia nyota wengine wa kizazi cha dhahabu cha Ubelgiji wanaocheza Ligi Kuu England
Kizazi cha dhahabu: Marouane Fellaini ni mmoja wa nyota wa kizazi cha dhahabu cha Ubelgiji, ambao kwa sasa wanacheza Ligi Kuu England