Na Mahmoud Zubeiry, Muscat
MARA ya mwisho Coastal Union ya Tanga kushinda taji ilikuwa ni mwaka 1988 walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, wakati huo ikiitwa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara.
Tangu wamekabidhiwa Kombe la ubingwa wa Bara, Coastal hawajawahi kukabidhiwa taji lingine kwa sababu hawajashinda mashindano yoyote mengine baada ya hapo.
Lakini jana, ikiwa ni miaka 26 baadaye, timu hiyo ilipewa taji, baada ya kukabidhiwa Ngao ya Urafiki na klabu ya
Fanja ya Oman, kutokana na kuzuru nchini hapa kucheza mechi ya kirafiki na klabu hiyo kigogo hapa.
Mwenyekiti wa Coastal, Hilal Hemed ‘Aurora’ alikuwa mwenye tabasamu pana wakati anapokea Ngao hiyo kutoka kwa Mwenyekiti wa Fanja, Saif Al Sumry. Mataji matamu, lakini lazima wayapiganie uwanjani.
MARA ya mwisho Coastal Union ya Tanga kushinda taji ilikuwa ni mwaka 1988 walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, wakati huo ikiitwa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara.
Tangu wamekabidhiwa Kombe la ubingwa wa Bara, Coastal hawajawahi kukabidhiwa taji lingine kwa sababu hawajashinda mashindano yoyote mengine baada ya hapo.
Fanja ya Oman, kutokana na kuzuru nchini hapa kucheza mechi ya kirafiki na klabu hiyo kigogo hapa.
Mwenyekiti wa Coastal, Hilal Hemed ‘Aurora’ alikuwa mwenye tabasamu pana wakati anapokea Ngao hiyo kutoka kwa Mwenyekiti wa Fanja, Saif Al Sumry. Mataji matamu, lakini lazima wayapiganie uwanjani.
![]() |
Kiungo wa Coastal Union ya Tangam Jerry Santo akimiliki mpira mbele ya kiungo wa Fanja ya Oman jana katika mchezo wa kirafiki uliofanyika Uwanja wa Fanja, Muscat, Oman, Fanja ilishinda 1-0. |
![]() |
Razack Khalfan nyuma akimdhibiti kiungo wa Fanja |
![]() |
Mshambuliaji wa Coastal akikabiliana na mchezaji wa Fanja |
![]() |
Hatari kwenye lango la Fanja |
![]() |
Haruna Moshi 'Boban' wa Coastal hapa alimpiga chenga moja hatari sana mchezaji huyu wa Fanja, kweli ujuzi hauzeeki |
![]() |
Wachezaji wa Fanja na Coastal wakigombea mpira |
![]() |
Jerry Santo kulia akimburuza kiungo wa Fanja |
![]() |
Wachezaji wa Coastal na baridi la Oman hadi kujifunika mablanketi benchi |
![]() |
Wachezaji, viongozzi na makocha wa Fanja na Coastal katika picha ya pamoja kabla ya mechi |
0 comments:
Post a Comment