Prince Nayef aliteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Oktoba mwaka jana [EPA]
|
MFALME mtarajiwa wa Saudi Arabia amefariki dunia kwa mujibu wa taarifa za Televisheni mida hii. Prince Nayef bin Abdulaziz Al Saud, ambaye alipewa madaraka hayo mwaka jana akiwa ana umri wa miaka 78, pia alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani wa nchi hiyo. Nayef hivi karibuni alikuwa nje ya nchi hiyo kwa matibabu na alifariki nje ya "mamlaka ya kifalme," imesema Televisheni ya said Al-Ekhbariyah, ikinukuu taarifa ya mamlaka. Taarifa ya leo kutoka kwa King Abdullah imesema kwamba Prince atazikwa kesho, ingawa hakutoa taarifa zaidi. Nayef alikuwa muumini wa maadili na asili ya nchi hiyo ambaye alipingana na mabadiliko katika muundo na mfumo wa nchi hiyo. Aliteuliwa kuwa Gavana wa Riyadh akiwa ana umri wa miaka 20 na alishikilia wadhifa huo kwa muda kabla ya kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani. Baada ya kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani kwa muda, mwaka 1975 alivuliwa wadhifa huo, wakati kaka yake Fahd alipoteuliwa kuwa Mfalme. Nayef alikuwa maarufu miongoni mwa serikali za Magharibi kwa jitihada zake za katika al-Qaeda. Mwanae, Muhammad bin Nayef, Naibu Waziri Mkuu, aliuawa mwaka 2009. |
Anambra: Legacy University, Okija sends SoS to Soludo over deplorable
access roads
-
From Aloysius Attah, Onitsha Management of Legacy University, Okija,
Anambra State, has made a passionate appeal for Gov. Soludo’s intervention
over t...
15 minutes ago
0 comments:
Post a Comment