• HABARI MPYA

    Monday, June 11, 2012

    PACQUIAO APIGWA KWA POINTI, LAKINI...











    Bradley akishangilia baada ya pambano


    BINGWA wa dunia uzito wa Welter anayetambuliwa na WBO, Manny Pacquiao usiku wa kuamkia jana amepoteza taji lake kwa mara ya kwanza baada ya kushindwa na Mmarekani, Timothy Bradley kufuatia uwamuzi wa kutatanisha mjini Las Vegas.


    Licha ya Pacquiao kupiga ngumi 94 ikiwa ni zaidi ya mpinzani wake, Mfilipino huyo alishindwa kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka saba baada ya majaji wawili kumpa Timothy Bradley pointi 115-113.
    Jaji mwingine alitofautiana na wenzake, akimpa ushindi Pacquiao wa pointi 115-113.
    Watazamaji wa pambano hilo hawakuridhika na uamuzi uliotangazwa na walizomea sana baada ya Bradley kutangazwa mshindi na hilo limezua uwezekano wa pambano la marudiano baadaye mwaka huu.
    "Nilihisi nimeshinda," alisema Bradley, ambaye hapo kabla alikuwa amechapisha tiketi kabambe za kuonyesha pambano la marudano kufanyika Novemba 10, mwaka huu.
    Bradley aliongezea; "Sidhani ni hodari kama wengi walivyomsifu. Makonde yake hayakua na nguvu."
    Pacquiao alichelewa kuingia ukumbini, lakini alipoingia alianza raundi ya kwanza kiuzembe uzembe ingawa alirusha ngumi tatu katika sekundi za mwisho wa raundi.
    Hadi kufikia raundi ya tano, Bradley alionekana kuzidiwa kutokana na maumivu ya jeraha la kidole cha mguu, ikionekana kuwa Pacquiao anaelekea kupata ushindi wa mteremko.
    Kwa upande wa Bradley alifanya vizuri katika raundi tatu za mwisho, lakini watazamaji hawakuridhika na hilo.
    Promota wa masumbwi, Bob Bradley alisema haiaminiki. Aliongezea kusema kuwa punde baada ya pambano kumalizika, alikwenda kwa Bradley na akamwambia, “Nimejitahidi kadri ya uwezo wangu, lakini sikuweza kumshinda mtu huyo.”
    Pacquiao mwenyewe alisema hakuweza kuamini matokeo hayo. Aliongezea kuwa; “Nimejitahidi, lakini naona juhudi zangu hazikutosha. Ngumi zake hazikunidhuru, mara nyingi ngumi zake ziliishia kwenye mikono yangu,” alisema Pacquiao.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PACQUIAO APIGWA KWA POINTI, LAKINI... Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top