• HABARI MPYA

    Tuesday, October 16, 2012

    NEMBO NYEKUNDU YA VODACOM MWIKO YANGA A, LAKINI RUKSA YANGA B

    Tangu msimu uliopita, Yanga imekuwa ikigoma kuvaa jezi za wadhamini wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Vodacom yenye rangi nyekundu. Msimu uliopita walibadilishiwa wakapewa jezi zenye nembo nyeusi na msimu huu pia wamegoma hadi sasa kuvaa jezi hizo kwa sababu ya doa jekundu. Lakini leo BIN ZUBEIRY alipotembelea mazoezi ya kikosi chao cha vijana chini ya umri wa miaka 20, maarufu kama Yanga B, alikuta baadhi ya wachezaji wamevaa jezi zenye kidoa chekundu, wakifanya mazoezi chini ya kocha wao, Salvatory Edward kwenye Uwanja wa Kaunda, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Kariakoo, Dar es Salaam. Je, kidoa chekundu cha Vodacom ni haramu kwa Yanga A tu, lakini Yanga B ruksa? 

    Wachezaji wa Yanga B wakifanya mazoezi Uwanja wa leo. Unaweza jezi zenye nembo nyekundu ya Vodacom

    Wachezaji wa Yanga B wakifanya mazoezi Uwanja wa leo mbele ya kocha wao, Salvatory Edward kulia. Unaweza jezi zenye nembo nyekundu ya Vodacom


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: NEMBO NYEKUNDU YA VODACOM MWIKO YANGA A, LAKINI RUKSA YANGA B Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top