• HABARI MPYA

    Tuesday, April 16, 2013

    ROONEY AWATULIZA 'UGONJWA WA MOYO' MAN UNITED


    MSHAMBULIAJI Wayne Rooney anataka mazungumzo ya mkataba mpya Manchester United mwishoni mwa msimu na amewaambia rafiki zake, hayuko tayari kuondoka Old Trafford kuhamia Paris St Germain.
    Mpachika mabao huyo wa United jana ilielezwa na Mshauri wa zamani wa PSG nchini Ufaransa kwamba dili la kumhamishia klabu ya Paris liko vizuri.
    Pamoja na hayo, inafahamika kwamba, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 anataka kukaa chini na United mwishoni mwa msimu huu kujadili kuongezewa mkataba ambao bado una miaka miwili.
    Enlarge Will he stay or will he go: Wayne Rooney wants to stay at Old Trafford but is reported to be a target for PSG
    Atabaki au ataondoka: Wayne Rooney anataka kubaki Old Trafford, lakini taarifa zinasema anatakiwa PSG

    Majadiliano na klabu hiyo ambayo muda si mrefu itavishwa taji la ubingwa wa Ligi Kuu England yanatarajiwa kuwa mazito.
    Rooney hatakuwa na shaka ya kuendelea kulipwa mshahara wa sasa wa Pauni 200,000 kwa wiki tangu Oktoba 2010 na United inaweza kumuongezea maslahi kidogo katika mkataba mpya.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ROONEY AWATULIZA 'UGONJWA WA MOYO' MAN UNITED Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top