• HABARI MPYA

    Tuesday, August 06, 2013

    RONALDO NA MESSI WACHONGANISHWA TENA NA UEFA

    Na Mahmoud Zubeiry, IMEWEKWA AGOSTI 6, 2013 SAA 4:31 USIKU
    MSHAMBULIAJI wa Real Madrid Cristiano Ronaldo atachuana na mpinzani wake mkuu, Lionel Messi wa Barcelona, zote za Hispania kuwania tuzo ya Mwanasoka Bora wa Ulaya.
    Taarifa ya UEFA iliyotumwa BIN ZUBEIRY leo, imesema kwamba, winga wa Bayern Munich, Franck Ribery ataungana na wakali hao katika orodha ya washindani watatyu wa mwisho katika tuzo hiyo ya msimu wa 2012/13.

    Overpriced? Gareth Bale, an £85m Real Madrid target, is only the seventh best player in Europe, according to the list
    Hata huyu? Gareth Bale, anatakiwa kwa dau la Pauni Milioni 85 na Real Madrid, naye hajaingia tatu bora
    Way off target: Robin van Persie came just tenth on the list
    Inauma: Robin van Persie aliishia 10 bora tu

    WALIOINGIA 10 BORA

    4) Robert Lewandowski (Poland) – Borussia Dortmund (Pointi 80)
    5) Arjen Robben (Uholanzi) – FC Bayern München (55)
    6) Thomas Müller (Ujerumani) – FC Bayern München (51)
    7) Gareth Bale (WalesL) – Tottenham Hotspur FC (48)
    8) Bastian Schweinsteiger (Ujerumani) – FC Bayern München (34)
    9) Zlatan Ibrahimović (Sweden) – Paris Saint-Germain FC (27)
    10) Robin van Persie (Uhoanzi) – Manchester United FC (24)
    Mfaransa huyo aliyetoa mchango mkubwa kwa Bayern kutwaa ubingwa wa Ulaya, anakuwa mchezaji wa kwanza kutoka nje ya klabu za Barcelona na Real Madrid kuingia fainali ya tuzo hiyo tangu mwaka 2011.
    Murgentina, Lionel Messi alishinda tuzo hiyo akifuatiwa na Andres Iniesta, mchezaji mwenzake wa Barcelona mwaka jana.
    Messi na mpinzani wake wa Real Madrid, mashambuliaji wa Ureno, Ronaldo wameingia fainali mara mfululizo miaka miwili iliyopita.
    Wachezaji wenzake watatu Ribery walioshinda mataji matatu na Bayern msimu uliopita- Thomas Mueller, Arjen Robben na Bastian Schweinsteiger waliingia 10 Bora iliyotangazwa mwezi uliopita.
    Mshindi ataamuliwa na jopo la Waandishi wa Habari wa soka kutoka nchi zote wanachama wa UEFA katika uchaguzi wa kura za wazi Agosti 29 wakati wa kutajwa kwa doroo ya Ligi ya Mabingwa  mjini Monaco.
    Hitman: Dortmund striker Robert Lewandowski was fourth on the list
    Muuwaji: Mshambuliaji wa Dortmund, Robert Lewandowski amekuwa wa nne kwenye orodha
    Wing wizard: Despite his winning goal in the Champions League Arjen Robben only came fifth on the list
    Mchawi wa Winga: Licha ya kufunga bao la ushindi lililoipa Bayern ubingwa wa Ulaya, Arjen Robben amepewa nafasi ya tano
    Another Munich man: Thomas Muller was sixth
    Mtu mwingine wa Munich: Thomas Muller amekuwa wa sita
    Quartet: Bastian Schweinseiger is the fourth and final player to appear on the list, at No 8
    Bastian Schweinseiger amekuwa wa nne na wa mwisho kwenye orodha, namba nane
    And finally: Zlatan Ibrahimovic was ninth, ahead of Robin van Persie
    Na wa mwisho: Zlatan Ibrahimovic amekuwa wa tisa, mbele ya Robin van Persie
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: RONALDO NA MESSI WACHONGANISHWA TENA NA UEFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top