• HABARI MPYA

    Sunday, August 04, 2013

    ROONEY AREJEA KIKOSINI MAN UNITED NA KUIWEZESHA TIMU KUSHINDA 3-0 DHIDI YA REAL

    IMEWEKWA AGOSTI 4, 2013 SAA 11:35 ALFAJIRI
    WACHEZAJI Wayne Rooney, Nani, Nemanja Vidic na Javier Hernandez wote walianza kikosini Manchester United katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Real Betis ambao mashabiki hawakuingia Uwanja wa Carrington.
    Mshambuliaji wa England, Rooney alicheza kipindi cha kwanza lakini hakuweza kufunga bao, mabingwa hao wa Ligi Kuu England wakishinda 3-0.
    Mchezo huo uliochezwa asubuhi ya jana kwenye Uwanja huo wa mazoezi wa United, ulikuwa wa kwanza kwa Rooney baada ya kuumia katika mechi ya kwanza ya ziara ya Mashariki ya Mbali mwezi uliopita.
    Checking in: Rooney arriving at the club's Carrington training ground on Friday
    Akiwasili: Rooney akiwasili kwenye Uwanja wa mazoezi wa Carrington juzi
    Back: Rooney will make his return against Real Betis in a closed doors friendly
    Amerudi: Rooney alicheza dhidi ya Real Betis 

    Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27, ambaye hajatulia, amepona maumivu ya nyama za paja aliyoyapata katika ziara ya Asia ya klabu hiyo na jana alionyesha yuko sawa akicheza dhidi ya timu hiyo ya La Liga. 
    Rooney anatarajiwa kuhama Old Trafford kutimkia Chelsea, ambao ofa yao ya pili ya Pauni Milioni 23 ilipigwa chini. 
    Anaweza kuwa na mazungumzo zaidi na kocha David Moyes wiki ijayo juu ya mustakabali wake wakati United ikijiandaa kwa mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya AIK mjini Stockholm. Lakini United inabaki na msimamo wake wa kumbakiza. 
    Return to action: Defender Nemanja Vidic tussles with George Ray of Crewe on Monday
    Amerudi kazini: Beki Nemanja Vidic akipambana na George Ray wa Crewe Jumatatu
    Closed doors: Vidic started in the friendly match behind closed doors on Saturday morning
    Milango imefungwa: Vidic alianza jana katika mchezo ambao ulichezwa milango imefungwa
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ROONEY AREJEA KIKOSINI MAN UNITED NA KUIWEZESHA TIMU KUSHINDA 3-0 DHIDI YA REAL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top