• HABARI MPYA

    Tuesday, August 06, 2013

    SUAREZ ATEMWA KIKOSI CHA LIERPOOR ZIARA YA NORWAY, SAFARI YA ARSENAL NINI?

    IMEWEKWA AGOSTI 6, 2013 SAA 3:32 USIKU
    MSHAMBULIAJI Luis Suarez ametemwa kwenye kikosi cha Liverpool kinachokwenda Valerenga kwa matatizo ya goti.
    Mpachika mabao huyo wa Uruguay, ambaye mustakabali wake haueleweki katika klabu hiyo, alitarajiwa kuwamo katika kikosi cha Brendan Rodgers kinachokwenda Norway kesho kwa mchezo wa kirafiki, lakini ameachwa Merseyside.
    Alipigwa picha akiondoka Uwanja wa mazoezi wa Liverpool, Melwood leo mchana, wakati wachezaji wengine wakiendelea na mazoezi.
    VIDEO Angalia David James: Suarez anahitaji kwenda
    Behind the wheel: Luis Suarez, leaving training on Tuesday, has been left out of Liverpool's trip to Norway
    Nyuma ya kioo: Luis Suarez, akiondoka mazoezini Jumanne, ameachwa kwenye kikosi cha Liverpool kinachokwenda Norway
    Luis Suarez leaves training
    Brendan Rodgers
    Steven Gerrard
    Hakuna dalili za Suarez: Brendan Rodgers na Steven Gerrard wakiwasili Uwanja wa Ndege wa Liverpool

    KIKOSI CHA LIVERPOOL KITAKACHOMENYANA NA VALARENGA

    Jones, Enrique, Toure, Alberto, Gerrard, Aspas, Coutinho, Assaidi, Henderson, Coates, Downing, Spearing, Lucas, Mignolet, Allen, Borini, Sterling, Kelly, Flanagan, Ibe, Wisdom.
    Suarez atakwenda kufanyiwa vipimo ili kujua uzito wa maumivu yake kama ataweza kusafiri kwenda Dublin Ijumaa kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa Liverpool wa kujipima dhidi ya Celtic Uwanja wa Aviva.
    Tangu amerejea kutoka mapumziko yake ya majira haya joto, Suarez amecheza akitokea benchi katika mechi dhidi ya Melbourne Victory, Thailand na Olympiakos Jumamosi iliyopita, huku akizungumziwa sana kuondoka Anfield.
    Unhappy: Luis Suarez is determined to leave Liverpool
    Hana furaha: Suarez anatarajiwa kuondoka Liverpool, na Arsenal iko mstari wa mbeke kumsajili
    Worrying time: Brendan Rodgers' plans for the coming season could be disrupted by Suarez
    Benchi: Brendan Rodgers anakwenda na timu yake Oslo kumenyana na Valarenga bila Suarez

    Liverpool imeendelea na msimamo wake wa kutotaka kumuuza Suarez, ingawa anahusishwa kwa kiasi kikubwa na Arsenal. 
    Timu ya Arsene Wenger imekwishatoa ofa mbili - moja ya Pauni Milioni 35, nyingine ya Pauni 40,000,001 - ambazo zote zimepigwa chini.
    Kukosekana kwake kesho hakutavuruga mipango ya Rodgers kuelekea msimu mpya, kwani Suarez atakosa mechi sita, akitumia adhabu yake iliyosalia kutokana na kumng'ata Branislav Ivanovic.
    Rodgers amemchukua pia Daniel Sturridge aliyerejea baada ya kupona kifundo cha mguu.
    Key man: It would come as a huge blow to Liverpool if Suarez were to leave
    Tegemeo: Itakuwa pigo kubwa kwa Liverpool ikiwa Suarez ataondoka
    New manager? Arsenal manager Arsene Wenger has had multiple bids rejected for the Liverpool striker
    Kocha wake mpya? Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amekwishatoa ofa mbili zilizopigwa chini Liverpool
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: SUAREZ ATEMWA KIKOSI CHA LIERPOOR ZIARA YA NORWAY, SAFARI YA ARSENAL NINI? Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top