• HABARI MPYA

    Saturday, October 05, 2013

    MOURINHO ASEMA HAJUTII KUMTOA KWA MKOPO LUKAKU, CHELSEA 'MUZIKI MNENE'

    IMEWEKWA OKTOBA 5, 2013 SAA 12:09 ASUBUHI
    KOCHA Jose Mourinho amesema hajutii kumtoa kwa mkopo mshambuliaji Romelu Lukaku kwenda Everton.
    Kocha huyo Chelsea alimshuhudia Lukaku akifunga mabao mawili dhidi ya Newcastle Jumatatu, akiongezea kwenye bao lake la kwanza alilofunga dhidi ya West Ham.
    Pamoja na kufunga mabao hayo matatu, lakini Mourinho amesema timu yake ni tofauti sana na ya Roberto Martinez.
    Watching eyes: Jose Mourinho was watching loan striker Romelu Lukaku's impressive display for Everton
    Macho makini: Jose Mourinho alimshuhudia mshambuliaji aliemtoa kwa mkopo Romelu Lukaku akicheza vizuri Everton
    From the spot: Lukaku scored two for the Toffees against Newcastle on Monday
    Kwa penalti: Lukaku aliifungia mabao mawili Toffees dhidi ya Newcastle Jumatatu

    Chelsea itakwenda kucheza na Norwich kesho, na Mourinho anatarajiwa kushusha kikosi kikali kilichoifunga Steaua mabao 4-0 mjini Bucharest Jumanne.
    Alipoulizwa kama anajuta kumtoa mchezaji huyo kwa mkopo, Mourinho alisema: "Hapana. NI kitu kimoja kuchezea Everton, na kingine kuchezea Chelsea,".
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MOURINHO ASEMA HAJUTII KUMTOA KWA MKOPO LUKAKU, CHELSEA 'MUZIKI MNENE' Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top