Na Zaituni Kibwana, Nairobi
WACHEZAJI wawili wa Eritrea wameripotiwa kutoroka wakati wakijiandaa na mchezo wa leo wa Kundi C, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge dhidi ya Uganda.
Ofisa wa Shirikisho la Soka Kenya (FKF) anayewaongoza Eritrea mjini hapa, Albert Shamola amesema kwamba wachezaji hao hawakuonekana baada ya kurejea kutoka uwanjani kuangalia mechi za jana.
Hii si mara ya kwanza kwa wachezaji wa Eritrea kutorokea nchi za watu wanapokwenda kwenye mashindano, kwani wamekwishawahi kufanya hivyo Tanzania pia mwaka 2010 na Uganda mwaka jana.
WACHEZAJI wawili wa Eritrea wameripotiwa kutoroka wakati wakijiandaa na mchezo wa leo wa Kundi C, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge dhidi ya Uganda.
Ofisa wa Shirikisho la Soka Kenya (FKF) anayewaongoza Eritrea mjini hapa, Albert Shamola amesema kwamba wachezaji hao hawakuonekana baada ya kurejea kutoka uwanjani kuangalia mechi za jana.
Hii si mara ya kwanza kwa wachezaji wa Eritrea kutorokea nchi za watu wanapokwenda kwenye mashindano, kwani wamekwishawahi kufanya hivyo Tanzania pia mwaka 2010 na Uganda mwaka jana.
0 comments:
Post a Comment