Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
KAMPUNI ya Azam Media Group itatoa zawadi ya king’amuzi kwa mchezaji bora wa kila mechi kuanzia hatua ya Robo Fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi, inayoendelea visiwani Zanzibar.
Robo Fainali zote zinachezwa leo kwenye viwanja viwili, Gombani, Pemba na Amaan, Zanzibar.
Kwenye Uwanja Gombani, mabingwa watetezi Azam FC watamenyana na Cloves Stars Saa 10:00 jioni, mechi itakayotanguliwa na mchezo mwingine wa hatua hiyo kati ya KMKM na URA ya Uganda.
Uwanja wa Amaan, Zanzibar mabingwa wa zamani wa michuano hiyo, Simba SC watamenyana na Chuoni ya Pemba kuanzia Saa 2:00 usiku, mechi itakayotangulia na mchezo mwingine kati ya KCC ya Uganda na Tusker ya Kenya.
Mgeni rasmi katika mchezo wa leo usiku Uwanja wa Amaan, anatarajiwa kuwa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi, ambaye ataongozana na Mjumbe wa Kamati yake ya Utendaji, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’.
Washindi wa mechi za leo watamenyana keshokutwa kusaka timu za kuingia Fainali Uwanja wa Amaan, wakati Fainali ya Kombe la Mapinduzi mwaka huu itachezwa Januari 13 Uwanja wa Amaan.
KAMPUNI ya Azam Media Group itatoa zawadi ya king’amuzi kwa mchezaji bora wa kila mechi kuanzia hatua ya Robo Fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi, inayoendelea visiwani Zanzibar.
Robo Fainali zote zinachezwa leo kwenye viwanja viwili, Gombani, Pemba na Amaan, Zanzibar.
Kwenye Uwanja Gombani, mabingwa watetezi Azam FC watamenyana na Cloves Stars Saa 10:00 jioni, mechi itakayotanguliwa na mchezo mwingine wa hatua hiyo kati ya KMKM na URA ya Uganda.
Uwanja wa Amaan, Zanzibar mabingwa wa zamani wa michuano hiyo, Simba SC watamenyana na Chuoni ya Pemba kuanzia Saa 2:00 usiku, mechi itakayotangulia na mchezo mwingine kati ya KCC ya Uganda na Tusker ya Kenya.
Mgeni rasmi katika mchezo wa leo usiku Uwanja wa Amaan, anatarajiwa kuwa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi, ambaye ataongozana na Mjumbe wa Kamati yake ya Utendaji, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’.
Washindi wa mechi za leo watamenyana keshokutwa kusaka timu za kuingia Fainali Uwanja wa Amaan, wakati Fainali ya Kombe la Mapinduzi mwaka huu itachezwa Januari 13 Uwanja wa Amaan.
0 comments:
Post a Comment