Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
KAMPUNI ya CXC Safaris & Tours itatoa zawadi kwa wachezaji watatu kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi, inayoendelea visiwani hapa, ambao ni mchezaji bora, mfungaji bora na kipa bora.
Mkurugenzi wa Kampuni ya CXC inayosifika kwa huduma nzuri za kitalii nchini, Charles Hamkah ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba ametoa ofa hiyo kwa Kamati ya Kombe la Mapinduzi, ili kunogesha michuano hiyo.
“Nimeamua kutoa ofa hii ili kunogesha mashindano haya, ambayo kwa kweli yanastahili kuungwa mkono zaidi ili yawe makubwa na bora zaidi,”alisema.
Hamkah amewaomba wadau wengi zaidi kujitokeza kupiga jeki zaidi mashindano hayo ambayo yanaendelea vyema tangu yaanzishwe mwaka 2007.
Kuhusu zawadi, Hamkah alisema atakutana na Kamati ya Kombe la Mapinduzi kujadiliana nayo viwango, lakini amesema zitakuwa zawadi nzuri na wachezaji watakaoshinda watazifurahia.
Hadi sasa, wachezaji sita wanachuana vikali katika ufungaji wa mabao, ambao ni Owen Kasuule, Feni Ali wote wa URA ya Uganda, ambao kila mmoja ana mabao matatu, Amri Kiemba Simba SC mabao mawili sawa na Brian Umony wa Azam FC, Mwinyi Mngwali wa Chuoni na Herman Waswa wa KCC.
Waliofunga bao moja kila mmoja ni Tony Odur, Stephen Bengo, Masiko Tom, William Waoro wa KCC ya Uganda, Hamisi Ali, Maulid Ibrahim Kapenta wa KMKM, Deus Kaseke, Paul Nonga wa Mbeya City, Ahmed Ali Omar, Mohamed Juma wa Cloves Stars, Joshua Oyoo, Ismail Dunga, Clifford Alwanga wa Tusker FC ya Kenya, Himid Mao, Kipre Tchetche wa Azam FC, George Thomas, Shaaban Moke wa Chuoni, Ekee Brayton Obina wa Ashanti na Abdallah Seif Bausi wa Spice Stars.
KAMPUNI ya CXC Safaris & Tours itatoa zawadi kwa wachezaji watatu kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi, inayoendelea visiwani hapa, ambao ni mchezaji bora, mfungaji bora na kipa bora.
Mkurugenzi wa Kampuni ya CXC inayosifika kwa huduma nzuri za kitalii nchini, Charles Hamkah ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba ametoa ofa hiyo kwa Kamati ya Kombe la Mapinduzi, ili kunogesha michuano hiyo.
“Nimeamua kutoa ofa hii ili kunogesha mashindano haya, ambayo kwa kweli yanastahili kuungwa mkono zaidi ili yawe makubwa na bora zaidi,”alisema.
![]() |
| Mfano wa kuigwa; Mkurugenzi wa CXC Safaris & Tours, Charles Hamkah atatoa zawadi kwa mfungaji bora, kipa bora na mchezaji bora Kombe la Mapinduzi |
Hamkah amewaomba wadau wengi zaidi kujitokeza kupiga jeki zaidi mashindano hayo ambayo yanaendelea vyema tangu yaanzishwe mwaka 2007.
Kuhusu zawadi, Hamkah alisema atakutana na Kamati ya Kombe la Mapinduzi kujadiliana nayo viwango, lakini amesema zitakuwa zawadi nzuri na wachezaji watakaoshinda watazifurahia.
Hadi sasa, wachezaji sita wanachuana vikali katika ufungaji wa mabao, ambao ni Owen Kasuule, Feni Ali wote wa URA ya Uganda, ambao kila mmoja ana mabao matatu, Amri Kiemba Simba SC mabao mawili sawa na Brian Umony wa Azam FC, Mwinyi Mngwali wa Chuoni na Herman Waswa wa KCC.
Waliofunga bao moja kila mmoja ni Tony Odur, Stephen Bengo, Masiko Tom, William Waoro wa KCC ya Uganda, Hamisi Ali, Maulid Ibrahim Kapenta wa KMKM, Deus Kaseke, Paul Nonga wa Mbeya City, Ahmed Ali Omar, Mohamed Juma wa Cloves Stars, Joshua Oyoo, Ismail Dunga, Clifford Alwanga wa Tusker FC ya Kenya, Himid Mao, Kipre Tchetche wa Azam FC, George Thomas, Shaaban Moke wa Chuoni, Ekee Brayton Obina wa Ashanti na Abdallah Seif Bausi wa Spice Stars.





.png)
0 comments:
Post a Comment