• HABARI MPYA

    Wednesday, January 08, 2014

    SIMBA ITAFURUKUTA KWA CHUONI LEO ZANZIBAR?

    Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
    MICHUANO ya Kombe la Mapinduzi, leo inaingia katika hatua ya Robo Fainali ka mechi nne kuchezwa kwenye viwanja viwili, Gombani, Pemba na Amaan, Zanzibar.

    Mnyama vitani: Simba SC itamenyana na Chuoni leo Uwanja wa Amaan

    RATIBA ROBO FAINALI MAPINDUZI

    KMKM Vs URA Saa 8:00 mchana (Gombani, Pemba)
    Azam FC Vs Cloves Stars Saa 10:00 jioni (Gombani, Pemba) 
    KCC Vs Tusker Saa 10:00 jioni (Amaan, Zanzibar)
    Simba SC Vs Chuoni Saa 2:00 Usiku (Amaan, Zanzibar).
    WANAOONGOZA KWA MABAO MAPINDUZI
    Owen Kasuule URA 3
    Feni Ali URA 3
    Amri Kiemba     Simba 2
    Brian Umony     Azam 2
    Mwinyi Mngwali Chuoni 2
    Herman Waswa KCC 2
    Kwenye Uwanja Gombani, mabingwa watetezi Azam FC watamenyana na Cloves Stars Saa 10:00 jioni, mechi itakayotanguliwa na mchezo mwingine wa hatua hiyo kati ya KMKM na URA ya Uganda.
    Uwanja wa Amaan, Zanzibar mabingwa wa zamani wa michuano hiyo, Simba SC watamenyana na Chuoni ya Pemba kuanzia Saa 2:00 usiku, mechi itakayotangulia na mchezo mwingine kati ya KCC ya Uganda na Tusker ya Kenya. 
    Mgeni rasmi katika mchezo wa leo usiku Uwanja wa Amaan, anatarajiwa kuwa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi, ambaye ataongozana na Mjumbe wa Kamati yake ya Utendaji, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’.
    Washindi wa mechi za leo watamenyana keshokutwa kusaka timu za kuingia Fainali Uwanja wa Amaan. 
    Fainali ya Kombe la Mapinduzi mwaka huu itachezwa Januari 13 Uwanja wa Amaan.
    Kilele cha michuano hiyo kinatarajiwa kufana kutokana na kwenda sambamba na sherehe za miaka 50 za mapinduzi ya Zanzibar.
    Azam itamenyana na Karafuu ya Pemba
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA ITAFURUKUTA KWA CHUONI LEO ZANZIBAR? Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top