Baadhi ya washiriki wa mbio za kujifurahisha
za”Vodacom 5 KM fun run”wakimaliza mbio zao nakujinyakulia zawadi mbalimbali.
 
 
Na Mwandishi Wetu, 
Moshi
Mbio za kujifurahisha za kilometa 5 za 
(Vodacom 5KM fun run) ambazo ni sehemu ya mbio za Kilimanjaro 
marathoni zimezidi kujizolea umaarufu kwa watu wengi wa rika 
tofauti kujitokeza kushiriki kwenye mbio hizo zilizofanyika jana/leo mjini Moshi 
mkoani Kilimanjaro.
Kwa mujibu wa Kaimu Mkuu wa kitengo cha Mahusiano wa 
kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania ambao ndio wadhamini wa mbio hizo, 
Rukia Mtingwa katika mbio za mwaka huu jumla ya watu 10,000 wamejitokeza 
kushiriki kwenye mbio hizo tofauti na makadirio ya kawaida ya 
kupata jumla ya washiriki 5000 ambacho ndicho huwa kiwango cha juu 
.
Mtingwa 
alisema wengi wa washiriki katika mbio hizo kwa mwaka huu 
zimetokana na uhamasishaji mkubwa uliofanywa na vyombo vya habari na 
mvuto wa mbio hizo ambazo huambatana na manjonjo mbalimbali Kutoka 
kwa washiriki wake na zawadi za kuvutia zinatolewa na Vodacom.
Pamoja na mafanikio hayo Mtingwa alisema wao kama 
wadhamini wamepata changamoto kubwa katika mbio hizo hasa kwa mwaka 
huu kutokana na wakimbiaji wazoefu kujitosa kushiriki kwenye mbio 
hizo badala ya kuwaachia watu wengine ambao riadha sio fani yao 
.
“Kwa kweli mwaka huu tumekumbana na changamoto hiyo ya 
wakimbiaji profession kushiriki kwenye fun run ambazo sisi tunaona 
ni maalum kwa watu ambao riadhi si fani yao kwahiyo kipindi kijacho endapo 
tutaendelea na udhamini wa mbio hizi itabidi tuifanyie kazi changamoto 
hii,”alisema Mtingwa .
Aidha Mtingwa alisema changamoto ya kujitokeza 
washiriki wengi kwao ni faraja kubwa na watajipanga kukubaliana na 
haki hiyo ili kuendana na mazingira ya ukubwa wa mbio 
hizo kadiri watu watakavyokuwa wakijitokeza.
Washindi wa mbio za jana/leo kwa upande wa 
wanaume ni Gailet Ismail ambaye alichukua na nafasi ya kwanza na 
kujinyakulia simu ya mkononi aina ya ZTE S- 501,muda wa maongezi wa Sh 20,000, 
modem ya intaneti pamoja na M-Pesa ya Sh 100,000.
Brazil Boay alichukua nafasi ya pili na kuzawadiwa simu 
,muda wa maongezi,modem ya intanert na M-Pesa ya Sh 80,000 wakati 
mshindi wa tatu alikuwa Fabiano Nelson ambaye naye alipata 
simu,muda wa maongezi,modem na M-Pesa ya Sh 60,000.
Na upande wa wanawake washindi walikuwa ni Jackline 
Sakilu,Catherine Iranga na Natalia Elisante ambao nao walijishindia zawadi sawa 
na zile walizopata wanaume , washindi wengi kuanzia nafasi wanne 
hadi 10 pamoja na wshiriki walioweza kumaliza mbio hizo nao walipata zawadi 
mbalimbali kutoka Vodacom.
Huo ni mwaka wa tano tokea Vodacom iwe 
mdhamini wa mbio za kilometa tano za kujifurahisha (Vodacom fun run) 
ambazo ni sehemu ya mbio maarufu za Kilimanjaro ambazo mwaka huu zimeadhimisha 
miaka 10 tokea kuanzishwa kwake .



.png)
0 comments:
Post a Comment