• HABARI MPYA

    Thursday, October 03, 2013

    SPURS YAENDELEZA UBABE ULAYA, YAIFUMUA TIMU YA ZAMANI YA ETO'O 2-0 URUSI

    IMEWEKWA OKTOBA 3, 2013 SAA 3:40 USIKU
    MABAO ya kipindi cha kwanza ya Jermain Defoe dakika ya 34 na Nacer Chadli dakika ya 39 yametosha kuipa ushindi wa 2-0 Tottenham katika Europa League usiku huu dhidi ya Anzhi Makhachkala nchini Urusi.
    Andre Villas-Boas aliwapumzisha wachezaji wake kadhaa wa kikosi cha kwanza katika mechi hiyo, lakini mabao mawili ndani ya dakika tano yalimpa faraja dhidi ya timu ya zamani ya Samuel Eto'o aliye Chelsea kwa sasa. 
    Ikitoka kuifunga Tromso 3-0 katika mchezo wa ufunguzi wa Kundi K, Spurs sasa imetimiza pointi sita na haijaruhusu nyavu zake kuguswa hata mara moja katika michuano hiyo. 
    Opener: Jermain Defoe (centre) is mobbed after scoring Tottenham's first goal
    La kwanza: Jermain Defoe (katikati) akipongezwa nawenzake baada ya kuifungia Tottenham bao la kwanza
    Kikosi cha Spurs kilikuwa: Lloris, Walker, Kaboul/Dawson dk71, Chiriches, Fryers, Holtby/Eriksen dk78, Dembele, Chadli, Sandro, Lamela/Sigurdsson dk72 na Defoe. 
    Anzhi: Pomazan, Angbwa/Gadzhibekov dk79, Tagirbekov, Adeleye, Ewerton, Jucilei, Ahmedov, Razak, Solomatin, Serderov/Yeschenko dk56 na Abdulavov/Traore dk45. 
    Loyal support: Spurs fans get behind their team in Russia
    Sapoti ya nguvu: Mashabiki wa Spurs wakiishangilia timu yao nchini Urusi
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: SPURS YAENDELEZA UBABE ULAYA, YAIFUMUA TIMU YA ZAMANI YA ETO'O 2-0 URUSI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top