• HABARI MPYA

    Thursday, December 12, 2013

    ARSENAL NA MAN CITY WANA KBARUA KIZITO LIGI YA MABINGWA...ANGALAU KIDOGO MAN UNITED NA CHELSEA

    BAADA ya kukamilikkwa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya, joto liliopo ni je klabu nne za England zilizofuzu zitakutana na timu gani katika hatua ya mtoano, inayojumuisha timu 16.
    Kuelekea droo hiyo Jumatatu mjini Nyon, BIN ZUBEIRY imetabiri timu ambazo zinaweza kukutana na klabu hizo za England katika michuano hiyo.
    Mbwa mkali zaidi: Cristiano Ronaldo atataka kuboresha rekodi yake ya mabao aliyoanza nayo katika hatua ya makundi akiwa Real Madrid

    Baada ya kuangukia katika nafasi ya pili kufuatia kipigo cha Napoli jana katika mchezo wa mwisho, Arsenal sasa inatarajiwa kuangukia kwa mpinzani mgumu kwenye hatua hiyo ya mtoano.
    Droo huwa inazingatia mambo kadhaa kama timu kutokutana na mpinzani iliyokuwa naye kundi moja na pia timu za nchi moja kutokutanishwa, huku timu zilizoongoza makundi zikicheza mechi za marudiano za mtoano nyumbani.
    Hiyo inamaanisha hakuna klabu za Ligi Kuu ya England zinazoweza kupambanishwa, lakini iko wazi The Gunners na Manchester City watakutana na wapinzani wagumu baada ya kushika nafasi za pili kwenye makundi yao.
    Fighting fit: Lionel Messi will return from injury to lead Barcelona's assault on the Champions League
    Anapambana kuwa fiti: Lionel Messi atarajea kutoka kwenye majeruhi kuiongoza Barcelona katika hatua ya mtoano

    Timu zote zinatazamiwa kutoepuka kukutana na vifofo wa Hispania, Real Madrid na Barcelona, wakati timu ya Arsene Wenger inaweza kukutana na mabingwa watetezi, Bayern Munich - City haiwezi kukutana na Bayern lakini inaweza kukutana na washindi wa pili wa msimu uliopita, Borussia Dortmund.
    Kwa Chelsea na Manchester United - ratiba ngumu kwao itakuwa ni kukutana na AC Milan. Pamoja na hayo, timu mbili zilizoongoza makundi zitapata timu hafifu kidogo katika hatua ya mtoano.
    ARSENAL
    Real Madrid
    PSG
    Bayern Munich
    Atletico Madrid
    Barcelona
    CHELSEA
    Bayer Leverkusen
    Galatsaray
    Olympiakos
    Zenit St Petersburg
    AC Milan
    MANCHESTER CITY
    Real Madrid
    PSG
    Dortmund
    Atletico Madrid
    Barcelona
    MANCHESTER UNITED
    Galatasaray
    Olympiakos
    Schalke
    Zenit St Petersburg
    AC Milan
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL NA MAN CITY WANA KBARUA KIZITO LIGI YA MABINGWA...ANGALAU KIDOGO MAN UNITED NA CHELSEA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top