• HABARI MPYA

    Monday, December 02, 2013

    IBRAHIMOVIC NA WENZAKE WA PSG WASHAMBULIWA KWA MAWE WAKIELEKEA UWANJANI, BASI LAVUNJWA VIOO

    MABASI ya timu za Paris Saint-Germain na Lyon za Ufaransa yote yalishambuliwa kwa mawe kabla ya mechi baina yao ya Ligue 1 Uwanja wa Parc des Princes mjini Paris jana jioni.
    Mabingwa PSG wamethibitisdha basi lao kushambuliwa na na kupasuliwa vioo wakati wakielekea uwanjani. Basi la Lyon inaaminika pia kupigwa mawe.
    Baada ya chaneli ya TV ya Ufaransa, Canal + kuonyesha picha za basi la PSG lilivyoathirika, ofisa mmoja akaiambia AFP: "Basi lilipigwa mawe na kioo cha mbele kulia kilipasuka.'
    Hatari kweli: Televisheni ya Ufaransa imeonyesha basi la PSG likiwa limepasuliwa kioo
    Up for it: Zlatan Ibrahimovic and his PSG team-mates emerge for their pre-match warm up after their bus was stoned on the way to the Parc des Princes
    Zlatan Ibrahimovic na wachezaji wenzake wa PSG wakipasha misuli moto baada ya kushuka kwenye basi lao lililopigwa mawe wakielekea Parc des Princes

    Nyota wakiwemo Zlatan Ibrahimovic, Thiago Silva na Edison Cavani inaaminika walikuwamo kwenye basi hilo wakisafiri na PSG, lakini wote walikuwemo kwenye kikosi cha kwanza cha kocha Laurent Blanc kilichowafumua wenyeji 4-0. 
    Cavani alifunga bao la kwanza kwa kichwa akiunganisha kona ya Lucas Moura dakika ya 36, kabla ya Ibrahimovic kufunga kwa penalti dakika ya 41. 
    Silva akafunga la tatu dakika ya 60 na Ibrahimovic akahitimisha karamu ya mabao kwa penalti tena dakika ya 83. 
    Flying high: Edison Cavani attempts an audacious scissor-kick during PSG's 4-0 win
    Edison Cavani akipiga mpira kikaretika
    Under pressure: Lyon's Yoann Gourcuff (right) is chased down by PSG duo Alex (left) and Marco Verratti (middle)
    Mchezaji wa Lyon, Yoann Gourcuff (kulia) akiwatoka wachezaji wa PSG, Alex (kushoto) na Marco Verratti (katikati)
    Too strong: Ibrahimovic celebrates scoring his first penalty of the night against Lyon
    Mtu wa nguvu: Ibrahimovic akishangilia baada ya kufunga penalti ya kwanza dhidi ya Lyon

    Tukio hilo lilitokea jirani na Chaville, linakuja kiasi cha wiki moja baada ya mashabiki wa Saint-Etienne kutolewa nje ya Uwanja wa Nice, Allianz Riviera baada ya watu wanane kujeruhiwa wakati wa mapambano baina ya mashabiki wa timu hizo.
    Mashabiki wa The Greens tangu wakati huo wamefungiwa kuingia kwenye mechi za ugenini kwa kipindi chote kilichobaki cha mwaka.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: IBRAHIMOVIC NA WENZAKE WA PSG WASHAMBULIWA KWA MAWE WAKIELEKEA UWANJANI, BASI LAVUNJWA VIOO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top