| Unakumbuka? Rais wa Simba SC, Evans Elieza Aveva akionyesha vidole vitatu wakati anakwenda kuchukua fomu za kugombea nafasi hiyo Mei 11, mwaka huu makao makuu ya klabu, Mtaa wa Msimbazi. Aveva alikuwa akionyesha vidole vitatu akimaanisha sera yake ni pointi tatu. Hata hivyo, timu hiyo imetoa sare mbili mfululizo katika Ligi Kuu, 2-2 na Coastal Union wiki iliyopita na 1-1 na Polisi Morogoro jana, zote Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Wazi Aveva anakabiliwa na changamoto ya kumaanisha sera yake hiyo kuanzia mechi ijayo. |
0 comments:
Post a Comment