Mrisho Ngassa (kushoto) akishangilia na wenzake, Simon Msuva kulia na Jerry Tegete baada ya kuifungia Yanga SC bao katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya. Mabao mengine ya Yanga yamefungwa na Simon Msuva na Amissi Tambwe, wakati bao pekee la Mbeya City limefungwa na Peter Mapunda.
0 comments:
Post a Comment