• HABARI MPYA

    Tuesday, June 05, 2012

    BANZA STONE KUTAMBULISHWA KESHO TWANGA PEPETA


    Banza akiimba na Twanga Pepeta, Leaders Club, Jumapili

    MWANAMUZIKI Ramadhani Masanja ‘Banza Stone’, kesho anatarajiwa kutambulishwa katika bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ katika onyesho la Usiku wa Mwafrika, kwenye ukumbi wa Club Billicanas, Dar es Salaam.
    Habari zilizofikia BIN ZUBEIRY kutoka ndani ya uongozi wa Twanga Pepeta, zimesema kwamba Banza amekwishamalizana na uongozi na kesho atatambulishwa rasmi Billicanas.
    Banza ambaye amekuwa akiimbia bendi ya Extra Bongo, alipanda jukwaa la Twanga Pepeta kwa mara ya kwanza Jumamosi kwenye ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni, Dar es Salaam wakati Extra Bongo ikitumbuiza ukumbi wa Meeda, Sinza.
    Banza Jumapili alipanda tena kwenye viwanja vya Leaders, Kinondoni na baada ya hapo akaingia kwenye mazungumzo na uongozi wa bendi hiyo na imeelezwa wamefikia makubaliano na Jenerali Mwana wa Masanja anarejea rasmi katika bendi iliyomuibua kimuziki, mwaka 1998. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BANZA STONE KUTAMBULISHWA KESHO TWANGA PEPETA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top