• HABARI MPYA

    Tuesday, June 05, 2012

    BREAKING NEWS; MOSIMANE ATIMULIWA BAFANA BAFANA


    South Africa's Pitso Mosimane shows frustration
    Mosimane
    KOCHA Pitso Mosimane amepoteza kazi katika timu ya taifa ya soka ya Afrika Kusini, baada ya kufukuzwa rasmi mchan wa leo.
    Mosimane aliondoka mara moja katika kambi ya timu, hoteli ya Royal Marang mjini Phokeng, Rustenburg baada ya kufukuzwa kwake kuthibitishwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Shirikisho la Soka Afrika Kusini (SAFA), Robin Peterson.
    Bafana Bafana imeshindwa imeshindwa kushinda hata mechi moja katika mechi saba, ikiwemo ya sare ya 1-1 na Ethiopia Jumapili.
    Nahodha wa zamani, Steve Komphela, ambaye aliteuliwa kuwa Msaidizi wa Mosimane, mapema Aprili, sasa atakuwa kocha wa muda wa timu hiyo.
    Komphela ataiongoza Bafana katika mechi ya kuwania tiketi ya kucheza Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil dhidi ya Botswana Jumapili, Juni 9 mjini Gaborone na mchezo wa kirafiki dhidi ya Gabon, Juni 15. 
    SAFA imeripotiwa kuandaa ofa kwa kocha wa Moroka Swallows, Gordon Igesund, ambaye kwa sasa yupo China na Dube Birds, lakini inasemekana hivi sasa yuko njiani kurejea nchini humo kujadili dili hilo la kuinoa timu ya taifa..
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BREAKING NEWS; MOSIMANE ATIMULIWA BAFANA BAFANA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top