• HABARI MPYA

    Friday, June 01, 2012

    ENGLAND YAFUNIKA VIBAYA EURO 2012


    Roberto Mancini - Vincent Kompany, Manchester City Premier League Victory Parade
    Getty
    LIGI Kuu ya England itawakilishwa vizuri katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya, Euro 2012 kwa asilimia 20 ya wachezaji wanaokwenda kwenye michuano hiyo kutoka kwenye klabu za Ligi hiyo ambao waling’ara msimu wa 2011-12.
    Uchambuzi uliofanywa na shirika la Sports Business Group huko Deloitte, umegundua asilimia 74 ya wachezaji wote 368 wa vikosi 16 vitakavyosafiri kwenda kwenye fainali hizo zinazoandaliwa kwa pamoja na Poland na Ukraine wanatoka ligi nyingine.
    Bundesliga ya Ujerumani ni ligi nyingine inayofuatia, ikiwa na asilimia 13 ya wachezaji kwenye michuano hiyo, ikifuatiwa na Hispania, La Liga yenye asilimia 9, Italia, Serie A na Urusi, Liga zote zikiwa na asilimia 9.
    Wakati wachezaji wengine watano zaidi wakicheza Ligi Daraja la Kwanza England, Championship msimu wa 2011-12, England pia ni taifa pekee, ambalo wachezaji wake wote 23 wanacheza ligi ya nchini mwao.
    Dan Jones, ofisa wa shirika hilo amesema: “Uwakilishi wa nguvu kutoka Ligi Kuu ya England katika Euro 2012 ni matokeo ya kuwa na ligi nzuri, inayohusisha wachezaji bora kutoka nchi tofauti duniani.
    Amesema pia wamegundua mapato ya Ligi Kuu yameongezeka kwa asilimia 12 hadi kufika pauni Bilioni 2.3 msimu wa 2010-11.
    Ongezeko la mapato hayo yanatokana na vyanzo vya kibiashara, huku ongezeko la asilimia 18 likipatikana hadi pauni Milioni 600, lakini pato kubwa zaidi kwa klabu za England linatokana na mapato ya matangazo, ambalo ni pauni Bilioni 1.18, huku Ligi Kuu ikiwapiku wapinzani wanaowakaribia, Bundesliga, kwa asilimia 40 ya mapato.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ENGLAND YAFUNIKA VIBAYA EURO 2012 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top