• HABARI MPYA

    Saturday, June 02, 2012

    NI KUFA NA KUPONA STARS V IVORY COAST ABIDJAN LEO


    Ngassa 'aliua' Tembo 2009
    HII itakuwa moja ya mechi kali kuzikutanisha timu za Magharibi mwa Afrika na Mashariki, wakati Ivory Coast watakapoikaribisha Tanzania leo mjini Abdijan.
    Huu utakuwa mchezo wa pili kwa kocha mpya wa Tanzania, Kim Poulsen baada ya sare ya bila kufungana na Malawi, Dar es Salaam na amejipanga kukabiliana na timu hiyo tishio zaidi Afrika kwa sasa.
    Kwa upande wa wenyeji, Sabri Lamouchi ni kocha mpya kabisa katika kikosi cha Tembo, kufuatia kufukuzwa kwa Francois Zahoui wiki iliyopita.
    Tanzania haijawahi kabisa kufuzu Fainali za Kombe la Dunia na ni miongoni mwa ndoto za Kim Poulsen anazotaka kutimiza akiwa kocha wa Taifa Stars.
    Kundi hilo C la kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 Brazil, linahusisha pia timu za Gambia na Morocco ukiondoa Ivory Coast na Tanzania.
    “Tunawaheshimu Ivory Coast kama timu ambayo inaundwa na wachezaji nyota duniani, kama Didier Drogba na Yaya Toure, na ambao wanacheza klabu kubwa Ulaya, lakini lazima wajiandae kupata wakati mgumu kutoka kwetu”, alisema Poulsen baada ya mazoezi yake ya kwanza mjini Abidjan jana.
    Drogba aliifunga Stars 2010 
    Mechi za karibuni kuzikutanisha timu hizo, ilikuwa mwaka 2009, katika michuano ya CHAN, ambayo Tanzania iliwafunga wenyeji 1-0, beo pekee Mrisho Ngassa wa Azam FC, enzi hizo akitokea Yanga na mwaka 2010, Ivory Coast walilipa kisasi Dar es Salaam katika mchezo wa kirafiki, bao pekee la Nahodha Didier Drogba.
    Wachezaji walio kambini mjini Abidjan kwenye kikosi cha Tembo Mkubwa ni makipa Ibrahim Kone na Badra Sandre, mabeki Kolo Toure, Emmanuek Eboue, Benjamin Angoua, Steve Gohouri, Brice Dja Djedje na Guy Demel, viungo Yaya Toure, Didier Zokora, Kafoumba Coulibaly, Marco Né, Moussa Kone, Romaric na Emerse Faé na washambuliaji Didier Drogba (Nahodha), Salomon Kalou, Serges Deble na Adama Bakayoko.
    Kwa upande wa Tanzania, nyota walio na timu Abidjan ni makipa Juma Kaseja (Nahodha), Mwadini Ally na Deogratius Munishi, mabeki Aggrey Morris, Amir Maftah, Erasto Nyoni, Kelvin Yondani, Waziri Salum, Shomari Kapombe na Juma Nyoso, viungo Mwinyi Kazimoto, Salum Abubakar, Shaaban Nditi, Edward Christopher, Mrisho Ngasa, Frank Domayo na washambuliaji Mbwana Samatta, John Bocco, Simon Msuya na Ramadhan Singano ‘Messi’.

    TAARIFA ZA MECHI:
    KUANZA: Saa 3.00 usiku (Afrika Mashariki, 11 jioni Ivory Coast)
    UWANJA: Stade Felix Houphouet-Boigny (watu: 35,000).
    REFA: Slim Jedidi (Tunisia).
    WASAIDIZI: Bechir Hassani (Tunisia) na Sherif Hassan (Misri).
    REFA WA AKIBA: Youssef Essrayri (Tunisia).



    MECHI NYINGINE ZA KUFUZU KOMBE LA DUNIA AFRIKA LEO
    15:00KenyavMalawiNairobi
    16:00Central African RepublicvBotswanaBangui
    16:30CameroonvCongo DRYaounde
    18:30Sierra LeonevCape VerdeFreetown
    18:30GambiavMoroccoBakau
    19:00SudanvZambiaKhartoum
    19:00Ivory CoastvTanzaniaAbidjan
    19:00TunisiavEquatorial GuineaMonastir
    20:00Burkina FasovCongoOuagadougou
    20:00SenegalvLiberiaDakar
    21:30AlgeriavRwandaBlida
    MECHI NYINGINE ZA KUFUZU KOMBE LA DUNIA AMERIKA KUSINI
    20:00UruguayvVenezuelaMontevideo
    22:10BoliviavChileLa Paz
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NI KUFA NA KUPONA STARS V IVORY COAST ABIDJAN LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top