• HABARI MPYA

    Saturday, June 02, 2012

    BOSI WA ANELKA ACHEZA NAMBA YA DROGBA CHINA


    MMILIKI wa klabu Shanghai Shenhua, Zhu Junb alianza kwa pamoja na Nicolas Anelka katika safu ya ushambuliaji ya timu hiyo katika mechi ya kirafiki hivi karibuni .

    Zhu Jun, owner of Shanghai Shenhua Zhu Jun, mmiliki wa Shanghai Shenhua akikosa bao
    Bilionea huyo wa Kichina, alicheza kwa dakika 45 kabla ya kutolewa mapumziko, Shenhua ikitoka sare ya 1-1 na CN Sports ya Argentina, katika mechi ambayo Anelka alikosa penalti kipindi cha pili. 
    Junb, mwenye umri wa miaka 45, alivaa jezi namba 11, lakini alipoteza nafasi kibao ambazo zinaweza kumshawishi kumletea Anelka pacha wake wa zamani, Drogba, ambaye kwa sasa yuko huru baada ya kubwaga manyanga Stamford Bridge.
    French striker Nicolas Anelka
    Kocha mchezaji Nicolas Anelka kazini
    Baada ya mechi hiyo, Zhu aliendelea kutoonyesha nia ya moja kwa moja ya kumchukua mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 34, mwenye Medali ya Dhahabu ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, akisema: 'Hilo ni swali zuri. Lakini siwezi kukujibu leo.’ 
    Anelka alijiunga na Shenhua Januari, mwaka huu na lazima aombe sana ombi lake la kuletewa Drogba likubaliwe 
    Pia, Junb anafikiria kumsajili na Fernando Torres…

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BOSI WA ANELKA ACHEZA NAMBA YA DROGBA CHINA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top