• HABARI MPYA

    Monday, June 04, 2012

    SIGOMBEI MAKAMU MWENYEKITI YANGA, BADO MCHANGA MIMI- BIN KLEB


    Abdallah Bin Kleb
    ABDALLAH Ahmed Bin Kleb, amesema kwamba ameombwa na wanachama wa klabu hiyo nchi nzima agombee nafasi ya Makamu Mwenyekiti, lakini amewaomba kwa sasa aanzie kwenye Ujumbe, ili kukusanya uzoefu zaidi, kwani kwa sasa anaamini bado hajapata uzoefu wa kutosha.
    Akizungumza na BIN ZUBEIRY usiku huu katika mahojiano maalum, Bin Kleb alisema kwamba baada ya makubaliano hayo wakapendekeza mtu mwingine wa kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti, wakati yeye anagombea Ujumbe.
    Bin Kleb alisema kwamba leo alikuwa kwenye msiba wa baba mkwe wake Davis Mosha na akapigiwa simu na Yussuf Manji akimtaarifu kumchukulia fomu ya kugombea Ujumbe wa Kamati ya Utendaji.
    Bin Kleb alisema Manji naye ana mpango wa kuchukua fomu ya kugombea Uenyekiti na na amepanga kufanya mambo makubwa mno katika Yanga, ikiwemo kujenga Uwanja wa kisasa na kuwekeza fedha nyingi katika klabu, ili iwe tishio kama Tout Puissant Mazembe iliyo chini ya milionea Moise Katumbi.
    “Mimi binafsi namuunga mkono Manji na ninaomba wana Yanga wote wamuunge mkono, kwa sababu ana mipango mizuri mno katika klabu,”alisema Bin Kleb, ambaye ameridhia kugombea Ujumbe baada ya kuchukuliwa fomu na Manji.
    Ingawa Katibu Mkuu wa Kamati ya Uchaguzi ya Yanga, Francis Kaswahili ameiambia BIN ZUBEIRY jioni hii kwamba Manji amewachukulia fomu Bin Kleb, Muhingo Rweyemamu kwa nafasi ya Ujumbe na Isaac Chanji kwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti, lakini mtu mmoja aliye ‘beneti’ na milionea huyo mwenye asili ya Kiasia, amesema Yussuf amechukua fomu leo ya kugombea Uenyekiti.
    Kama Manji naye amechukua fomu, idadi ya waliochukua fomu hadi sasa inafika watu 11, baada ya awali Ayoub Nyenzi kuchukua fomu ya kugombea Makamu Mwenyekiti, Jumanne Mwamenywa, John Jambele, Peter Haule, Gaudicius Ishengoma, Abdallah Sharia na Saleh Abdallah, wote Ujumbe.
    Uchaguzi wa Yanga unaokuja baada ya Wajumbe wengi wa Kamati ya Utendaji iliyoingia madarakani mwaka juzi, kujiuzulu akiwemo Mwenyekiti, Wakili Lloyd Baharagu Nchunga unatarajiwa kufanyika Julai 15, mwaka huu na mwisho wa zoezi la kuchukua ni keshokutwa 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIGOMBEI MAKAMU MWENYEKITI YANGA, BADO MCHANGA MIMI- BIN KLEB Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top