• HABARI MPYA

    Monday, June 04, 2012

    UHURU SULEIMAN AOTA MBAWA YANGA, ASAINI MKATABA MPYA SIMBA HADI 2014


    Ameota mbawa Jangwani; Uhuru Suleiman ameongeza mkataba Simba

    KIUNGO hodari, Uhuru Suleiman Mwambungu, au Robinho amesaini mkataba mpya wa miaka miwili na klabu yake, Simba SC na hivyo kuzima ndoto za Yanga waliokuwa wanamtaka mchezaji huyo kumpata.
    Uhuru, aliyetua Simba misimu miwili iliyopita akitokea Mtibwa Sugar ya Morogoro, iliyomtoa Coastal Union ya Tanga, ameiambia BIN ZUBEIRY leo jioni kwamba ameongeza mkataba wa miaka miwili na klabu yake.
    “Kaka nimesaini mkataba mpya wa miaka miwili na hivi ninavyozungumza na wewe nimekuja kwetu Mbeya kijijini kabisa kuchukua baraka za wazee, kisha nirudi kazini na nguvu mpya,”alisema Uhuru.
    Uhuru hakutaka kuwazungumzia Yanga, kwa sababu amesema hakuwahi hata kukaa nao meza moja zaidi ya kusikia tetesi kwamba wanamtaka.
    “Nilisikia Yanga walikuwa wananitaka, ila kwa kweli mimi naona wamechelewa, kwa sababu nimekwishaongeza mkataba na timu yangu,”alisema.
    Wachezaji wengine wa kikosi cha kwanza Simba msimu huu, ambao mikataba yao imeisha ni mabeki Juma Nyosso na Juma Jabu, ambao nao wanahusishwa na mpango wa kuhamia kwa mahasimu wa jadi, Yanga. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: UHURU SULEIMAN AOTA MBAWA YANGA, ASAINI MKATABA MPYA SIMBA HADI 2014 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top