• HABARI MPYA

    Monday, June 04, 2012

    BREAKING NEWS: MANJI ACHUKUA FOMU YANGA LEO


    Manji

    YUSSUF Mehboob Manji, leo ametinga makao makuu ya Yanga, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani na kuwachukulia fomu za kugombea uongozi, wanachama watatu, katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Julai 15, mwaka huu mjini Dar es Salaam.
    Kwa kitendo hicho cha kuingia Jangwani na kuchukua fomu, wengi wamedhani Manji amechukua fomu za kugombea mwenyewe na tetesi zimeenea Dar es Salaam kwamba anagombea Uenyekiti.
    Lakini Katibu Mkuu wa Kamati ya Uchaguzi ya Yanga, Francis Kaswahili ameiambia BIN ZUBEIRY jioni hii kwamba Manji amewachukulia fomu wanachama watatu, ambao ni Abdallah Bin Kleb na Muhingo Rweyemamu kwa ajili ya nafasi za Ujumbe wa Kamati ya Utendaji na Isaac Chanji kwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti.
    Lakini bado kuna uvumi kwamba Manji mwenyewe wakati wowote atachukua fomu ya kuwania Uenyekiti, ingawa awali ilielezwa anamuunga mkono Francis Kifukwe awanie nafasi hiyo.
    Kuchukua fomu kwa wajumbe hao watatu, kunafanya idadi ya waliochukua fomu hadi sasa kufika 10, baada ya awali Ayoub Nyenzi kuchukua fomu ya kugombea Makamu Mwenyekiti, Jumanne Mwamenywa, John Jambele, Peter Haule,
    Gaudicius Ishengoma, Abdallah Sharia na Saleh Abdallah, wote Ujumbe.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BREAKING NEWS: MANJI ACHUKUA FOMU YANGA LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top