• HABARI MPYA

    Tuesday, October 16, 2012

    HAKUNA UFISADI KATIKA USAJILI SIMBA, HANS POPPE AKANUSHA MADAI YA MRWANDA

    Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe kushoto akimkabidhi jezi ya Simba Daniel Akuffo baada ya kusajiliwa. Katikati ni Makamu Mwenyekiti wa Simba SC, Geoffrey Nyange 'Kaburu'

    Na Mahmoud Zubeiry
    SIMBA SC imesema kwamba hakuna ‘ufisadi’ wa aina yoyote katika zoezi la usajili katika klabu hiyo kutokana na utaratibu mzuri uliowekwa na mshambuliaji Danny Mrwanda aliachwa kwa sababu ya dau kubwa alilotaka.
    Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amekanusha kwa nguvu zote madai kwamba wachezaji huombwa ‘twenty percent’ ili kusajiliwa na kusistiza kwamba Mrwanda alishindana na klabu hiyo ndiyo maana akaachwa.
    “Alitaka dau kubwa, baadaye akakubali dau tulilotaka kumpa, baadaye tena ajaka anatutajia timu nyingine inamtaka, sisi tukamuambia basi nenda kwenye hiyo timu nyingine, ndivyo tulivyoachana naye huyo bwana,”alisema Hans Poppe.
    Mrwanda alijiunga tena na Simba na Juni mwaka huu, akitokea Vietnam alipokuwa anacheza soka ya kulipwa, lakini baada ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, Julai mwaka huu akatemwa.
    Baada ya kutemwa Mrwanda, akasajiliwa mshambuliaji Daniel Akuffo kutoka Ghana ambaye hata hivyo, kocha Mserbia Milovan Cirkovick haridhishwi na uwezo wake.
    Mrwanda aliwahi kumzungumzia Akuffo na kusema tatizo ni twenty percent, jambo ambalo sasa Hans Poppe anakanusha.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: HAKUNA UFISADI KATIKA USAJILI SIMBA, HANS POPPE AKANUSHA MADAI YA MRWANDA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top